Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 3:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Basi, nikatambua kwamba hakuna jambo linalokuwa bora zaidi kwa mwanadamu kufanya kuliko kufurahia kazi yake, kwa sababu amepangiwa hivyo. Nani anayeweza kumujulisha mwanadamu yale yatakayokuwa kisha kufa kwake?

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 3:22
24 Iomraidhean Croise  

Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari. Wakizarauliwa, yeye haoni kabisa.


Mupumbafu anasema maneno mengi. Mwanadamu hajui yatakayokuwa, wala yale yatakayotukia nyuma yake.


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Nikachukia jasho yote niliyotoa hapa chini ya jua, kuona kwamba ilinipasa nimwachie mutu ambaye atatawala nyuma yangu.


Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu,


Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?


Katika siku za kufanikiwa ukuwe na furaha. Katika siku za hasara ufikiri juu ya jambo hili: Mungu amefanya hiyo ya kwanza iambatane na ya pili kusudi mwanadamu asipate kujua mambo yatakayotukia nyuma yake.


Basi, mimi ninasifu furaha, kwa maana hapa chini ya jua hakuna kitu kinachokuwa kizuri zaidi kuliko kula na kunywa na kujifurahisha. Haya ndiyo mutu anayoweza kufanya anapotoa jasho katika muda wa maisha yake aliyojaliwa na Mungu chini ya jua.


Hajui ni kitu gani kitakachotukia nyuma, maana ni nani anayeweza kumujulisha yatakayotukia nyuma?


Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.


Upendo wao, chuki zao na tamaa zao, vyote vimetoweka pamoja nao, wala hawatashiriki tena katika kitu chochote hapa chini ya jua.


Lakini wewe, ee Danieli, ujiendee, upumzike katika kaburi, na wakati huo utakapotimia, utafufuka na kupata zawadi yako.


Basi musijisumbue kwa ajili ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Kila siku ina masumbuko yake inayoitoshelea.


Mutavikula mbele ya Yawe, Mungu wenu, pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua. Mutavikula ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi katika miji yenu.


Huko, mutakula mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mutafurahi ninyi pamoja na watu wa nyumba zenu kwa ajili ya mafanikio yenu Yawe, Mungu wenu, aliyowabarikia.


“Yawe, Mungu wenu aliwabariki katika kila njia, lakini ninyi hamukumutumikia kwa moyo wa furaha na shangwe.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan