20 Wote wanakufa na kwenda kwa nafasi moja. Wote wametoka katika mavumbi na wote watarudi katika mavumbi.
Isimaeli alikuwa na umri wa miaka mia moja makumi tatu na saba alipokufa na kukutana na wazee wake.
Kisha kuishi maisha marefu na ya fanaka, akakufa na kukutana na wazee wake.
Kwa jasho la uso wako utajipatia chakula, mpaka utakaporudi katika udongo, maana ulitwaliwa katika udongo. Wewe ni mavumbi na utarudi katika mavumbi.”
Lakini mutu anakufa na ule ndio mwisho wake. Akisha kutoa roho, anabakiliwa na nini tena?
Mutu akikufa anaweza kuishi tena? Siku zangu zote za kazi ningekungoja mpaka wakati wa kufunguliwa ufike.
Kama kuzimu kukiwa nyumba yangu, na makao yangu yako kule katika giza,
Basi, mutu akiangamia hainui mukono? Mutu akiwa tabani haombi musaada?
viumbe vyote vingeangamia kabisa, naye mwanadamu angerudi katika mavumbi.
Kama vile wingu linavyofifia na kutoweka, ndivyo nao watu wanavyoshukia kuzimu bila kurudi.
Mungu anajua jinsi tulivyoumbwa; anajua kwamba sisi ni mavumbi.
Ukiwageuzia mugongo, wanaogopa; ukiondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi ndani ya mavumbi walimotoka.
Hayo ndiyo yanayowapata wanaojitumainia kwa upumbafu, ndio mwisho wa wale wanaojivunia mali zao.
mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.
Nani anayejua, basi, kama kweli roho ya mutu inapanda juu, na roho ya nyama inashuka chini ndani ya udongo?
Ingawa mutu huyo ataishi miaka elfu mbili, lakini hafurahii maisha, basi yeye ni kama yule mutoto. Wote wawili wanakwenda fasi moja.
Afazali kwenda kwenye kilio, kuliko kwenda kwenye karamu, kwa sababu inawapasa wenye kuwa wazima kukumbuka kwamba kifo kinawangojea sisi wote.
Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.
Wengi wa wale ambao wamekwisha kufa, watafufuka; wengine watapata uzima wa milele, na wengine watapata haya na kuzarauliwa milele.
Ukisha kuiona, utakufa na kukutana na wazee wako, kama vile ndugu yako Haruni alivyokutana nao,