Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 3:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Mwisho wa mwanadamu na mwisho wa nyama ni mumoja. Jinsi mwanadamu anavyokufa ndivyo nyama anavyokufa. Wote wanapumua namna ileile; mwanadamu si bora kuliko nyama. Yote ni bure.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 3:19
18 Iomraidhean Croise  

Sisi wote tutakufa. Sisi ni kama maji yaliyomwangika chini ambayo hayawezi kuzoleka. Lakini Mungu hataki Abusaloma akufe sasa au aendelee kuishi mbali naye.


Ukiwageuzia mugongo, wanaogopa; ukiondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi ndani ya mavumbi walimotoka.


Ingawa walisema kwamba udongo ni wao, lakini ni makaburi ndiyo nyumba zao hata milele, ni makao yao vizazi hata vizazi.


Mwanadamu hadumu katika utajiri wake; anakufa tu kama nyama.


atakwenda kukutana na babu zake waliomutangulia kufa, ambao hawawezi kuona tena mwangaza.


Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!


Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.


Mwenye hekima anaona anakokwenda, lakini mupumbafu anatembea katika giza. Hata hivyo, ninajua vilevile kwamba mwisho wao wote wawili ni mumoja.


Maana hakuna anayemukumbuka mwenye hekima, wala anayemukumbuka mupumbafu, maana katika siku zinazokuja wote watasahaulika. Maana mwenye hekima anakufa sawasawa na mupumbafu!


Afazali kwenda kwenye kilio, kuliko kwenda kwenye karamu, kwa sababu inawapasa wenye kuwa wazima kukumbuka kwamba kifo kinawangojea sisi wote.


Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.


maana mwisho uleule unawapata wenye haki na waovu, wazuri na wabaya, wanaohesabiwa kuwa safi na wachafu, wenye kutoa sadaka na wasiotoa sadaka. Mutu muzuri ni sawa tu na mwenye zambi, na mwenye kuapa si tofauti na asiyeapa.


Watu hawa wakikufa kifo cha kawaida, au wakipatwa na hasara kama watu wengine, basi mujue kwamba Yawe hakunituma.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan