Hapana hata kidogo! Sherti Mungu ajulikane kuwa mwenye ukweli, na kila mutu kuwa mwongo, kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ee Mungu, sherti ujulikane kuwa mwenye haki katika masemi yako. Nawe ushinde wakati unaposhitakiwa.”
Walimu hawa wa uongo ni kama nyama wasiokuwa na akili ambao wanazaliwa tu kwa kunaswa na kuchinjwa. Wao wanasema vibaya juu ya mambo yote wasiyojua. Wataangamizwa kufuatana na ubaya wao wenyewe.