Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 3:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Basi, nikasema ndani ya moyo wangu: “Mungu atawahukumu watu wa haki hata vilevile na waovu, maana amepanga wakati kwa kila jambo na kwa kila kazi.”

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 3:17
32 Iomraidhean Croise  

Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”


mbele ya Yawe kwa sababu anakuja. Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki, na mataifa kwa uaminifu wake.


Mushangilie mbele ya Yawe, maana anakuja kutawala dunia. Atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kama vile inavyofaa.


Basi, nikafikiri nikisema: “Nimejipatia hekima nyingi zaidi kupita wote waliopata kutawala Yerusalema mbele yangu. Kweli, ninajua hekima na maarifa ni nini.”


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.


Basi, nikawaza: “Ngoja nijitumbukize katika raha, nijifurahishe.” Lakini, niligundua kwamba hiyo nayo ni bure.


Kuna muda kwa kila kitu, na wakati kwa kila jambo katika dunia:


Kweli, kila kitu kina wakati wake na njia yake, ingawa mwanadamu anapatwa na tatizo kubwa.


Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Akanijibu: Danieli, ujiendee, maana maneno haya ni siri na yamefungwa kwa kutiwa muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


Na zaidi ya hii Baba hahukumu hata mutu mumoja, lakini amemupa Mwana uwezo wote wa kuhukumu,


Yesu akawajibu: “Si kazi yenu kutambua siku wala nyakati Baba yangu alizopanga kwa mamlaka yake mwenyewe.


Kwa maana amekwisha kupanga siku atakapohukumu dunia kwa haki, kwa njia ya mutu mumoja, yule aliyemuweka kwa kazi ile. Naye amehakikisha mambo hayo kwa kumufufua mutu yule.”


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


Wandugu, si lazima kwenu niwaandikie jambo lolote juu ya wakati wala saa ambayo mambo hayo yatatokea.


Watu wa mataifa mengine walikasirika, lakini kasirani yako imetokea. Sasa ni wakati wa kuhukumu waliokufa, nao wakati wa kuwapa waliokutumikia zawadi, ndio manabii wako, na wote wanaoheshimu jina lako, wakubwa na wadogo. Ni wakati wa kuangamiza wale wanaoharibu dunia!”


Akamukamata yule nyoka mukubwa, ndiye yule nyoka wa zamani, anayeitwa “Mwovu” au “Shetani” na kumufunga kwa muda wa miaka elfu moja.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan