Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 3:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mungu amefanya kila kitu kikuwe kizuri kwa wakati wake. Ameweka ndani ya moyo wa mwanadamu mawazo juu ya muda usiokuwa na mwisho, lakini mutu hawezi kuelewa mwanzo na mwisho wa matendo ya Mungu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 3:11
19 Iomraidhean Croise  

Mungu akaona kwamba kila kitu alichofanya ni kizuri kabisa. Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya sita.


Unaweza kuvumbua siri za Mungu na kujua ukomo wa Mungu Mwenye Uwezo?


Mungu Mwenye Uwezo asiyeweza kufikiwa na mutu, uwezo na haki yake ni mukubwa. Amejaa haki wala hapotoshi sheria hata kidogo.


yeye anayetenda mambo makubwa yasiyochunguzika, anayetenda maajabu yasiyohesabika.


Ee Yawe, matendo yako ni mengi sana! Umeyafanya kwa hekima yote! Dunia imejaa viumbe vyako!


Yawe ameumba kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya maangamizi.


Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.


Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.


Mufikiri vema juu ya kazi ya Mungu. Ni nani anayeweza kunyoosha kitu Mungu alichokunja?


Nimeyapima yale yote kwa hekima; nikajisemesha: “Ninataka kuwa mwenye hekima!” Lakini hekima iko mbali sana nami.


Nimetambua jambo hili moja: kwamba Mungu aliwaumba wanadamu wenye usawa, lakini wao wenyewe wamejitafutia matatizo.


lakini hataelewa kazi ya Mungu inayofanyika chini ya jua. Mutu anaweza kutoa jasho sana lakini hataelewa. Wenye hekima wanaweza kujidai kwamba wanajua, lakini, kwa kweli, hawajui.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika miiba, ni mufano wa wale wanaosikia Neno la Mungu, lakini masumbuko ya dunia hii na udanganyifu wa mali vinasonga lile neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


Nao watu wakashangaa sana na kusema: “Mambo anayofanya ni mazuri kweli. Anawawezesha hata viziwi wasikie, nao wabubu wapate kusema.”


Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan