Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kuna muda kwa kila kitu, na wakati kwa kila jambo katika dunia:

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 3:1
12 Iomraidhean Croise  

Lakini Elisha akamwambia: “Unafikiri roho yangu haikukuwa pamoja nawe wakati mutu yule alipotoka ndani ya gari lake na kuja kukutana nawe? Huu ndio wakati wa kupokea feza na nguo, mashamba ya mizeituni na mizabibu, kondoo na ngombe au watumishi na wajakazi?


Wakati alipokuwa katika taabu, akamwomba Yawe, Mungu wake rehema. Akajinyenyekeza sana mbele ya Mungu wa babu zake.


Kutoa jibu zuri kunafurahisha; neno linalofaa kwa wakati wake ni jema sana!


Kwanza fanya kazi zako inje na kutayarisha kila kitu katika shamba. Kisha jenga nyumba yako.


Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.


Kwa hiyo, nikachukia maisha, maana yote yanayotendeka chini ya jua yalinisikitisha. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.


Basi, nikasema ndani ya moyo wangu: “Mungu atawahukumu watu wa haki hata vilevile na waovu, maana amepanga wakati kwa kila jambo na kwa kila kazi.”


Katika siku za kufanikiwa ukuwe na furaha. Katika siku za hasara ufikiri juu ya jambo hili: Mungu amefanya hiyo ya kwanza iambatane na ya pili kusudi mwanadamu asipate kujua mambo yatakayotukia nyuma yake.


Naye Mufalme wa Misri, mumupange jina hili: Mwenye domo ya bure!


Na asubui munapoona kwamba mawingu ni meusi munasema kwamba mvua itanyesha. Munajua kutambua hali ya mawingu, lakini hamuwezi kujua vitambulisho vya nyakati hizi.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan