Muhubiri 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Nilijikusanyia feza na zahabu kutoka hazina za wafalme na toka katika majimbo, nami nilipata waimbaji wanaume na wanawake, na wahabara wanaotamaniwa.
Kisha malkia akamupa mufalme zaidi ya kilo elfu ine za zahabu, marasi nyingi sana na mawe ya bei kali. Hakuna aliyeweza hata kidogo kumuletea mufalme Solomono marasi mengi sana sawa yale malkia wa Seba aliyomuletea.
Vyombo vyote vya kunywa divai vya mufalme Solomono vilikuwa vya zahabu, na vyombo vyote vilivyokuwa katika Nyumba ya Pori ya Lebanoni vilikuwa vya zahabu safi; hakuna kilichotengenezwa kwa feza maana madini ya feza haikuhesabiwa kuwa kitu wakati ule.
Mufalme Daudi na viongozi wa Walawi, wakachagua wazao wa Asafu, wa Hemani, na wa Yedutuni, kwa kuongoza katika kazi ya kutabiri kwa kutumia vinubi, na vinanda na matoazi. Haya ndiyo majina ya wale waliochaguliwa kwa kuongoza ibada, pamoja na aina ya kazi iliyofanywa na kila kikundi:
Wana wake wote walipiga muziki kwa matoazi, vinanda na vinubi, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe wakiwa chini ya uongozi wa baba yao. Asafu, Yedutuni na Hemani walikuwa chini ya uongozi wa mufalme.
Solomono alitumia miti hiyo kwa kutengeneza madari ya nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme, na tena kwa kutengeneza vinubi na vinanda vya waimbaji. Mpaka wakati ule miti hiyo ilikuwa haijaonekana katika inchi ya Yuda.
Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?
mukisikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, munapaswa kuinama chini na kuabudu sanamu ya zahabu mufalme Nebukadneza aliyosimamisha.
Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha.