Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Nilinunua watumwa, wajakazi, na wengine wakazaliwa katika nyumba yangu. Nilikuwa na mali mengi, makundi ya ngombe na kondoo wengi kuliko mutu yeyote aliyenitangulia kukaa Yerusalema.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 2:7
16 Iomraidhean Croise  

Wakati ule, Abramu alikuwa ametajirika sana. Alikuwa na makundi ya nyama, feza na zahabu.


Abramu alipopata habari kwamba mwipwa wake amekamatwa kuwa mufungwa, akatoka na watu wake mashujaa mia tatu na kumi na wanane waliozaliwa katika nyumba yake, akawafuatilia waadui mpaka Dani.


Angalia, haujanijalia mutoto. Mutumwa aliyezaliwa ndani ya nyumba yangu ndiye atakayekuwa murizi wangu!”


Mufalme Mesha wa Moabu alikuwa mufugaji wa kondoo, na kila mwaka alilipa kodi kwa mufalme wa Israeli wana-kondoo elfu mia moja na manyoya ya kondoo wengine elfu mia moja.


Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.


Kati ya wazao wa watumishi wa Solomono, waliorudi kutoka katika uhamisho, kulikuwa wazao wa watu hawa: Sotayi, Hasofereti, Peruda, Yala, Darkoni, Gideli, Sefatia, Hatili, Pokereti-Hazebaimu, Ami.


Watumishi wote wa hekalu na wazao wa watumishi wa Solomono waliorudi kutoka katika uhamisho walikuwa watu mia tatu makumi kenda na wawili.


Ukoo za wazao wa watumishi wa mufalme Solomono waliorudi kutoka katika uhamisho zilikuwa ukoo za: Sotayi, Sofereti, Perida, Yala, Darkoni, Gideli, Sefatia, Hatili, Pokereti-Hazebaimu, Amoni.


Alikuwa na mali, kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, ngombe elfu moja, punda dike mia tano, na watumishi wengi sana. Yeye alikuwa wa heshima kuliko watu wote kule upande wa mashariki.


Katika miaka ya Yobu iliyofuata, Yawe alimubariki zaidi kuliko hata alivyokuwa amemubariki pale mbele. Basi Yobu akakuwa na kondoo elfu kumi na ine, ngamia elfu sita, ngombe elfu mbili na punda dike elfu moja.


Lakini kama mutumishi yule akijisemesha mwenyewe kwamba bwana wake anakawia kurudia; na halafu anaanza kuwapiga watumishi wenzake, wanaume na wanawake, naye anakula na kunywa na kulewa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan