Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 2:3
22 Iomraidhean Croise  

Yakobo akamujibu: “Umri niliojaliwa kama musafiri ni miaka mia moja na makumi tatu. Miaka hiyo imekuwa michache na iliyojaa mateso, tena haijafikia hesabu ya miaka wazee wangu waliyoishi kama wasafiri.”


Mutu akikufa anaweza kuishi tena? Siku zangu zote za kazi ningekungoja mpaka wakati wa kufunguliwa ufike.


apate divai ya kumuchangamusha, mafuta ya muzeituni ya kumwangarisha, na mukate wa kumupa nguvu.


Divai inaleta mazarau na kileo kinaleta ugomvi; yeyote anayevutwa navyo hana hekima.


Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.


Chakula ni kwa ajili ya kujifurahisha, divai inachangamusha maisha, na feza inasababisha hayo yote.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu,


Kama Mungu anamupa mutu utajiri na mali na kumujalia wakati wa kuyafurahia, basi mwanadamu ashukuru na avifaidie hivyo alivyojipatia kwa jasho lake. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.


Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?


Inakupasa ushike neno la kwanza na la pili vilevile; maana anayemutii Mungu atayaepuka yote.


Hata hivyo, nilikusudia kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na maana ya mambo yanayokuwa, na vilevile kujua kwamba uovu ni upumbafu na kwamba upumbafu ni wazimu.


Basi, mimi ninasifu furaha, kwa maana hapa chini ya jua hakuna kitu kinachokuwa kizuri zaidi kuliko kula na kunywa na kujifurahisha. Haya ndiyo mutu anayoweza kufanya anapotoa jasho katika muda wa maisha yake aliyojaliwa na Mungu chini ya jua.


“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.


Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.


Lakini muzabibu ukajibu: ‘Munazani ninaweza kuacha shuguli yangu ya kuzalisha divai ambayo inafurahisha miungu na wanadamu, niende kujisumbua kuitawala miti?’


Abigaili aliporudi kwake, alimukuta Nabali akifanya karamu kubwa katika nyumba yake kama ya kifalme. Nabali alikuwa akifurahi sana ndani ya moyo maana alikuwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia neno lolote mpaka asubui.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan