Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 2:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 2:26
24 Iomraidhean Croise  

Yawe akamwambia Noa: “Ingia ndani ya chombo wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wa kizazi hiki, nimekuona wewe peke yako kuwa mutu wa haki mbele yangu.


Lakini ile roho inayokuwa ndani ya mutu, ile pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo, ndiyo inayomwezesha mwanadamu kufahamu.


Ni nani aliyemujulisha kwarara kujaa kwa muto Nili au aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?


Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda mabaya mbele yako. Hivi uamuzi wako ni wa haki, hukumu yako haipotoki.


Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.


Maana Yawe anawapa watu hekima; katika kinywa chake kunatoka maarifa na ufahamu.


Anayeongeza mali yake kwa mazidio na kulipisha faida, anamukusanyia mwingine mwenye kuwahurumia wamasikini.


Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.


Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!


maana usipojaliwa na Mungu, hauwezi kupata chakula wala kujifurahisha.


Mimi nimeiona kazi ambayo mwanadamu amepewa na Mungu.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Mpaka sasa hamujaomba kitu kwa jina langu. Muombe, nanyi mutapewa, na furaha yenu itakuwa kubwa kabisa.


Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan