Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 2:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu,

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 2:24
22 Iomraidhean Croise  

Watu wa Yuda na wa Israeli walikuwa wengi kama muchanga wa bahari, nao walikuwa wakikula, wakikunywa, na kufurahi.


Sasa murudi kwa nyumba mufanye sherehe, mukule vyakula na kunywa divai nzuri, lakini mukumbuke kuwapelekea wale ambao hawana kitu cha kutosha; maana leo ni siku takatifu kwa Bwana wetu. Musihuzunike kwa sababu furaha Yawe anayowajalia itawapa nguvu.”


Kila kitu macho yangu yalichokitamani nilikipata. Moyo wangu sikuunyima raha yoyote. Moyo wangu ulifurahia mambo niliyotenda, na hii ilikuwa zawadi ya jasho langu.


maana usipojaliwa na Mungu, hauwezi kupata chakula wala kujifurahisha.


Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.


Basi, nikatambua kwamba hakuna jambo linalokuwa bora zaidi kwa mwanadamu kufanya kuliko kufurahia kazi yake, kwa sababu amepangiwa hivyo. Nani anayeweza kumujulisha mwanadamu yale yatakayokuwa kisha kufa kwake?


Basi, haya ndiyo niliyotambua: jambo zuri na lenye kufaa kwa mwanadamu ni kula, kunywa na kufurahia matunda ya jasho anayotoa hapa chini ya jua, siku zile chache za maisha aliyojaliwa na Mungu, maana hivi ndivyo alivyopangiwa.


Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?


Mungu anamujalia mutu utajiri, mali na heshima, hata hakosewi kitu chochote anachotamani, lakini hamupi uwezo wa kuvifurahia vitu hivyo. Pahali pake, mugeni fulani atavifaidia. Hayo nayo ni bure. Ni jambo la mateso mabaya.


Basi, mimi ninasifu furaha, kwa maana hapa chini ya jua hakuna kitu kinachokuwa kizuri zaidi kuliko kula na kunywa na kujifurahisha. Haya ndiyo mutu anayoweza kufanya anapotoa jasho katika muda wa maisha yake aliyojaliwa na Mungu chini ya jua.


Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai; mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali! Kesho itakuwa kama leo, tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.


Ni lazima muniheshimu mimi kwa matendo yenu. Musiponisikiliza nitawaletea laana. Vitu vyote munavyopewa kwa mahitaji yenu nitavilaani. Na kweli nimekwisha kuvilaani, kwa sababu hamushuguliki hata kidogo na maagizo yangu.


Ingawa vile hakuacha kujijulisha kwa njia ya kutenda mema. Anawanyeshea mvua toka mbingu, anawapa mavuno kwa wakati wake, anawapa chakula na kuwajaza na furaha.”


Ikiwa ni kwa nia ya kimutu, nimepigana na nyama wakali wa pori katika Efeso, jambo lile limenifalia nini? Kama wafu hawafufuki, basi: “Tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.”


Huko mutafurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi kati yenu kwa sababu hawana sehemu wala urizi kati yenu.


Mutavikula mbele ya Yawe, Mungu wenu, pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua. Mutavikula ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi katika miji yenu.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan