Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 2:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Maisha yake yote yamejaa taabu, na jasho yake ni mahangaiko matupu. Hata usiku akili yake haipumziki! Hayo nayo ni bure.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 2:23
20 Iomraidhean Croise  

Kisha akamwambia yule mwanaume: “Wewe umemusikiliza muke wako na kula matunda ya muti ambayo nilikuamuru usikule. Basi, udongo umelaaniwa kwa sababu yako. Kwa jasho utajipatia toka humo chakula chako, siku zote za maisha yako.


Yakobo akamujibu: “Umri niliojaliwa kama musafiri ni miaka mia moja na makumi tatu. Miaka hiyo imekuwa michache na iliyojaa mateso, tena haijafikia hesabu ya miaka wazee wangu waliyoishi kama wasafiri.”


Usiku ule, mufalme hakupata usingizi. Basi, akaamuru kitabu cha Mambo ya Siku cha matukio ya kila siku, kiletwe, nacho kikasomwa mbele yake.


Mutu anazaliwa na mwanamuke, ana siku chache, na taabu nyingi.


Lakini mwanadamu anazaliwa apate taabu, kama vile cheche za moto zinavyoruka juu.


Munajisumbua bure kuamuka asubui mapema na kuchelewa kwenda kupumzika magaribi, mujipatie chakula kwa jasho lenu. Mungu anatimiza mahitaji ya wapendwa wake hata wanapolala.


Muchana na usiku mukono wako ulinilemea; nguvu zangu zikakwisha, kama maji yanavyokauka wakati wa kipwa.


Utujalie sasa miaka mingi ya furaha, kama ulivyotupa miaka mingi ya shida na taabu.


Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.


Maana katika kuwa na hekima nyingi kuna wasiwasi; na anayeongeza maarifa zaidi anaongeza huzuni zaidi.


Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.


Tena, nimeona jambo moja ovu sana chini ya jua: mutu alijikusanyia mali, ikakuwa hatari kwake.


Basi, haya ndiyo niliyotambua: jambo zuri na lenye kufaa kwa mwanadamu ni kula, kunywa na kufurahia matunda ya jasho anayotoa hapa chini ya jua, siku zile chache za maisha aliyojaliwa na Mungu, maana hivi ndivyo alivyopangiwa.


Kila mara nilipojitoa kwa kujua hekima na kuona yanayotendeka hapa katika dunia, nilitambua kwamba mutu anaweza kukaa macho muchana na usiku,


Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mulango wa lile pango. Mufalme akapiga muhuri wake mwenyewe na ule wa wakubwa wake, kusudi uamuzi uliotolewa juu ya Danieli usibadilishwe.


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan