Mungu Mwenye Nguvu awajalie kupata huruma mbele ya mutu yule, awaachie yule ndugu yenu mwingine na Benjamina warudi pamoja nanyi. Kwa upande wangu, ikinipasa kupotelewa na wana wangu, basi!”
Tena, ni nani anayejua kwamba atakuwa mwenye hekima au atakuwa mupumbafu? Hata hivyo, yeye atarizi yote niliyofanya kwa kutoa jasho na kutumia hekima yangu hapa chini ya jua. Hayo nayo ni bure.
Maana, wakati mwingine, mutu ambaye amefanya kazi kwa kutumia hekima, akili na maarifa yake, anamwachia mutu mwingine afurahie matunda ya kazi ambayo hakuitoshea jasho. Hayo nayo ni bure. Ni jambo baya sana.