Ee Yawe, mukono wako uwafukuze kati ya watu, tukio lao likuwe kutengana na wanaokuwa wazima. Uwashibishe kwa akiba uliyowawekea, watoto wao nao washibe na kuacha sehemu, wawaachie hata na wajukuu wao.
Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.
Maana, wakati mwingine, mutu ambaye amefanya kazi kwa kutumia hekima, akili na maarifa yake, anamwachia mutu mwingine afurahie matunda ya kazi ambayo hakuitoshea jasho. Hayo nayo ni bure. Ni jambo baya sana.
Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.
Basi, nikatambua kwamba hakuna jambo linalokuwa bora zaidi kwa mwanadamu kufanya kuliko kufurahia kazi yake, kwa sababu amepangiwa hivyo. Nani anayeweza kumujulisha mwanadamu yale yatakayokuwa kisha kufa kwake?
Kama Mungu anamupa mutu utajiri na mali na kumujalia wakati wa kuyafurahia, basi mwanadamu ashukuru na avifaidie hivyo alivyojipatia kwa jasho lake. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Furahia maisha pamoja na muke wako unayemupenda muda wote wa maisha yako ya bure ambayo Mungu amekujalia hapa chini ya jua, maana hilo ndilo ulilopangiwa katika maisha, katika kutoa jasho yako hapa chini ya jua.
Kwa kadiri ya zawadi Mungu aliyonipatia, kama vile fundi wa kujenga mwenye hekima, niliweka musingi. Na sasa, mutu mwingine anajenga juu yake. Lakini inafaa kila mutu aangalie vizuri namna anavyojenga.