naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”
Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.
Jua lilipotokea, Mungu akaleta upepo mukali kutoka upande wa jangwa, jua likamuchoma sana Yona juu ya kichwa, karibu azimie. Akatamani kufa, akisema: Ni vizuri kwangu kufa kuliko kuishi.