Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 2:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Maana hakuna anayemukumbuka mwenye hekima, wala anayemukumbuka mupumbafu, maana katika siku zinazokuja wote watasahaulika. Maana mwenye hekima anakufa sawasawa na mupumbafu!

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 2:16
17 Iomraidhean Croise  

Mufalme alimwomboleza Abeneri akisema: “Imekufikia namna gani ee Abeneri kufa kama mupumbafu?


upepo unapovuma juu yake yanatoweka, na mahali yalipokuwa hapaonekani tena.


kimwezeshe aendelee kuishi siku zote, bila kuona kaburi.


Wema wako unatajwa ndani ya kaburi, au uaminifu wako katika shimo la kuangamia?


Kisha, Yosefu akakufa, vilevile na wandugu zake na kizazi kile chote.


Basi, kukatokea mufalme mwingine kule Misri ambaye hakumujua Yosefu.


Hekima ya mwenye akili inamwonyesha njia yake, lakini upumbafu wa wapumbafu unawadanganya wenyewe.


Hakuna mutu anayekumbuka mambo ya zamani, wala atakayekumbuka yatakayotukia kisha.


Mwenye hekima anaona anakokwenda, lakini mupumbafu anatembea katika giza. Hata hivyo, ninajua vilevile kwamba mwisho wao wote wawili ni mumoja.


Basi, nikasema ndani ya moyo wangu: “Yatakayomupata mupumbafu yatanipata na mimi vilevile. Kwa nini, basi, nimekuwa na hekima zaidi?” Nikasema ndani ya moyo wangu: “Hayo nayo ni bure.”


Basi mutu mwenye hekima ana faida zaidi kuliko mupumbafu? Na mutu masikini anapata faida gani akijua namna ya kuishi?


Afazali kwenda kwenye kilio, kuliko kwenda kwenye karamu, kwa sababu inawapasa wenye kuwa wazima kukumbuka kwamba kifo kinawangojea sisi wote.


Tena, nimeona waovu wakizikwa, watu ambao walizoea kuingia na kutoka pahali patakatifu, na kusifiwa katika muji uleule walimotenda maovu yao. Hayo nayo ni bure.


Katika muji ule, kulikuwa masikini mumoja mwenye hekima ambaye, kwa hekima yake, aliokoa muji ule. Lakini hakuna mutu aliyemukumbuka yule masikini kisha.


Maana, wanaoishi wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui kitu chochote. Hawana malipo tena. Hakuna ukumbusho juu yao, wamesahauliwa kabisa.


Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan