Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 12:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 watu wanaogopa mupando na kutishwa katika njia, muti wa lozi unachanua maua yake meupe, mapanzi hayawezi kuruka, hakuna hamu tena, mwanadamu anaelekea kwenye makao yake ya milele, waombolezaji wanasambaa katika njia,

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 12:5
19 Iomraidhean Croise  

Lakini baba yake akamujibu: “Mwana wangu hatakwenda nanyi. Ndugu yake amekwisha kufa, naye peke yake ndiye aliyebaki. Mimi ni muzee mwenye imvi. Ikiwa kijana huyu atapatwa na hasara yoyote katika safari mutakayofanya basi, mutaniua kwa huzuni.”


Kama mutamupeleka huyu vilevile kutoka kwangu, akipatwa na hasara, basi mutanishusha katika kaburi nikiwa muzee mwenye huzuni.’


na akiona kwamba kijana hayupo pamoja nasi, atakufa! Hivyo sisi watumishi wako tutamwua baba yetu kwa huzuni.


Kati yetu kuna wazee wenye hekima, wenye miaka mingi kuliko baba yako.


Kama kuzimu kukiwa nyumba yangu, na makao yangu yako kule katika giza,


Kweli! Ninajua utanipeleka tu katika kifo, pahali wote wanaoishi watakapokutana.


Usiniachilie, ee Mungu, nitakapokuwa muzee mwenye imvi nyingi, kusudi nivitangazie vizazi vitakavyokuja nguvu yako.


Kuwa na imvi za uzee ni taji la utukufu; zinapatikana kwa maisha ya haki.


Utukufu wa vijana ni nguvu zao. Uzuri wa wazee ni kichwa chenye imvi.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Mimi nitabaki yuleyule hata katika uzee wenu; hata katika wakati wenu wa imvi mimi nitawabeba. Nilifanya hivyo kwanza, nitafanya hivyo tena. Nitawabeba ninyi na kuwaokoa.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: Yeremia, unaona nini? Nami nikasema: Ninaona tawi la muti wa uangalivu ambao maua yake yamekwisha kuchanua.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mufikiri na kuwaita wanawake waombolezaji; muwaite wanawake wanaoelewa nyimbo za kilio.


Unapokuwa mbele ya muzee unapaswa kusimama kwa kumupa heshima yake, nawe umwogope Mungu wako. Mimi ni Yawe.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan