Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 12:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 12:14
17 Iomraidhean Croise  

Lakini muogope azabu, chuki yenu isiwaletee kifo. Mujue kwamba kutakuwa hukumu!


Umefanya hayo yote nami nimenyamaza. Unazani kwamba mimi ni kama wewe? Lakini sasa nitakukaripia, nitakugombeza waziwazi.


Maovu yetu umeyaweka mbele yako; zambi zetu za siri ziko wazi mbele yako.


mbele ya Yawe kwa sababu anakuja. Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki, na mataifa kwa uaminifu wake.


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Basi, nikasema ndani ya moyo wangu: “Mungu atawahukumu watu wa haki hata vilevile na waovu, maana amepanga wakati kwa kila jambo na kwa kila kazi.”


“Basi musiwaogope watu wale. Hakuna kitu chochote kinachofichwa kitakachokosa kuvumbulikana wala hakuna siri itakayokosa kujulikana.


“Ninawaambia wazi kwamba kwa Siku ya hukumu, watu watasamba kila neno lisilokuwa na maana walilosema.


na kutoka ndani ya makaburi yao. Waliotenda mema watafufuka na kupata uzima, lakini waliotenda mabaya watafufuka na kuhukumiwa.


Hiyo ndiyo itakayotokea siku ile Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya watu kwa njia ya Yesu Kristo, kama vile Habari Njema yangu inavyosema.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan