Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 12:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 12:13
27 Iomraidhean Croise  

Malaika akamwambia: “Usinyooshe mukono wako juu ya kijana wala usimufanyie jambo lolote! Sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu, maana haukuninyima hata mwana wako wa pekee.”


Timiza maagizo ya Yawe, Mungu wako, ufuate njia zake na kushika masharti yake, amri zake, maagizo yake na maamuzi yake kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa. Kwa hiyo, utafanikiwa katika kila jambo unalofanya na kokote unakoenda.


Kisha Mungu akamwambia mwanadamu: Sikia! Kumwogopa Bwana ndiyo hekima, na kujitenga na uovu ndiyo maarifa.


Kumwogopa Yawe ni musingi wa hekima; wote wanaotii amri zake wanajaliwa akili. Sifa zake zinadumu milele.


Anajibia mahitaji yao wote wanaomwabudu; anasikia kilio chao na kuwaokoa.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Kumwogopa Yawe ni musingi wa maarifa, lakini wapumbafu wanazarau hekima na mafundisho.


Kumwogopa Yawe kunaongoza kwenye uzima; anayemwogopa anajaliwa pumziko la kutoshelea, wala hatapatwa na ubaya wowote.


Moyo wako usiwaonee wivu wenye zambi, lakini endelea kumwogopa Yawe siku zote.


Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.


Ninajua kwamba jambo lolote Mungu analotenda linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa. Mungu amefanya mambo yakuwe hivyo kusudi wanadamu wamwogope yeye.


Usishangae ukiona katika inchi wamasikini wanagandamizwa, wananyimwa haki na sheria zao. Kila mwenye cheo anayewatesa wamasikini yupo chini ya mukubwa mwingine, na juu ya hao wote kuna wakubwa zaidi.


Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?


Inakupasa ushike neno la kwanza na la pili vilevile; maana anayemutii Mungu atayaepuka yote.


Wenye zambi wanatenda maovu mara mia. Hata hivyo, wanaendelea kuishi. Lakini, mimi ninajua kwamba itakuwa heri kwa wanaomwogopa Mungu, kwa sababu ya woga wao.


Anayetii amri hatapata hasara, na mwenye hekima atajua kwamba kuna wakati wa hukumu.


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.


“Sasa, enyi Waisraeli, Yawe, Mungu wenu, anataka nini kwenu? Yawe, Mungu wenu, anataka mumwogope, mufuate njia zake zote, mumupende, mumutumikie Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wote na kwa roho yenu yote,


Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.


juu ya siku ile ambayo mulisimama mbele ya Yawe, Mungu wenu, kule Horebu, ndio Sinai, aliponiambia: ‘Muwakusanye hao watu mbele yangu, niwaambie maneno yangu kusudi wajifunze kuniogopa mimi siku zote za maisha yao, na kuwafundisha watoto wao kufanya hivyo’.


Musiongeze chochote katika amri ninazowapa, wala musipunguze kitu. Mushike amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa.


Wakati wote munapokuwa wazima, mutapaswa kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kutii masharti yote na amri ninazowapa ninyi na wazao wenu kusudi mupate kuishi maisha marefu.


Muwaheshimu watu wote. Muwapende wandugu zenu waamini. Mumwogope Mungu, mumuheshimu mufalme.


Kisha sauti ikasikilika toka kwenye kiti cha kifalme ikasema: “Mumusifu Mungu wetu ninyi watumishi wake wote, ninyi wote munaomuheshimu, wakubwa na wadogo!”


Basi, ninyi mumutii Yawe na kumutumikia kwa uaminifu, kwa moyo wenu wote. Mukumbuke yale mambo makubwa aliyowatendea.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan