Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 12:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ukumbuke Muumba wako siku za ujana wako wakati hazijafika siku mbaya wala haijakaribia miaka utakaposema: “Sina furaha katika vitu hivyo.”

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 12:1
40 Iomraidhean Croise  

Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, akamufanikisha sana. Yosefu akakuwa anakaa katika nyumba ya bwana wake Mumisri.


Yule mukubwa wa kifungo hakujishugulisha tena na kitu chochote Yosefu alichopewa kwa maana Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kufanikisha kila kitu alichofanya.


Lakini Barzilayi akamwambia mufalme: “Niko tena na miaka mingi ya kuishi ndipo niende nawe mufalme mpaka Yerusalema?


Mimi leo nina umri wa miaka makumi nane. Niko na uwezo wa kutambua yanayokuwa mazuri na yale yasiyokuwa mazuri? Mimi mutumishi wako ninaweza tena kutambua onjo ya kile ninachokula au kunywa? Nitaweza tena kutambua uzuri wa sauti za waimbaji wanaume au wanawake? Kwa nini mimi mutumishi wako nikuwe muzigo wa zaidi kwako bwana wangu mufalme?


Watu wote wa Israeli watafanya kilio na kumuzika. Lakini, ni huyo tu wa jamaa ya Yeroboamu atakayezikwa, maana ni yeye tu wa jamaa ya Yeroboamu aliyepata kupendezwa na Yawe, Mungu wa Israeli.


Ninaogopa kwamba mara tu nitakapoondoka, Roho wa Yawe atakunyanyua na kukupeleka pahali nisipopajua! Nikienda kumwambia Ahabu kwamba uko hapa, naye akikutafuta na asikupate, ataniua mimi, ingawa mimi mutumishi wako ninamwogopa Yawe tangu ujana wangu.


Ukiwa pahali popote unapofanya kazi, mara utakaposikia baragumu, kimbilia kwetu. Mungu wetu atatupigania.”


Ningepata faida gani katika mikono yao, watu ambao nguvu zao zilikuwa zimewaishia?


Usiku ninakukumbuka, ee Yawe, na kushika sheria yako.


Hata simba wakali wanakosewa na kusikia njaa, lakini wanaomutafuta Yawe hawakosewi chochote kizuri.


Roho yangu itafurahi kama mwenye kushiba minofu yenye mafuta, kwa shangwe nitaimba sifa zako.


Muda wa maisha yetu ni miaka makumi saba, au tukikuwa wenye afya, miaka makumi nane; lakini yote ni shida na taabu! Siku zinapita mbio, nasi tunatoweka!


Umufundishe mutoto njia anayopaswa kufuata, naye hataiacha hata katika uzee.


Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.


Ondoa mahangaiko ndani ya moyo wako, ujikinge usipate maumivu katika mwili kwa sababu ujana na nguvu vinapita mbio.


Gawa sehemu moja kwa watu saba hata wanane, maana, haujui hasara itakayofika katika dunia.


Mutu akiishi miaka mingi, afurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kwamba siku mbaya zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.


Katika njia ya maamuzi yako tunakungojea ee Yawe; tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.


Ni vizuri kwa mutu kujifunza uvumilivu tangu wakati wa ujana wake.


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Wageni wamenyonya nguvu zake, wala yeye mwenyewe hajui; imvi zimejaa juu ya kichwa chake, lakini yeye mwenyewe hana habari.


kwa maana atahesabiwa kuwa mutu mukubwa mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kinywaji kikali, na atajazwa na Roho Mutakatifu tangu kuzaliwa kwake.


Lakini Yesu akawaita na kusema: “Muwaache watoto wadogo wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.


Na ninyi wababa musiwakasirikishe watoto wenu. Lakini muwalee na kuwaonya, mukiwatolea mashauri yanayotoka kwa Bwana.


Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye anayewapa uwezo wa kupata utajiri. Anafanya hivyo kwa kuimarisha agano alilofanya na babu zenu mpaka leo.


Tena, tangia utoto wako unajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupatia hekima kusudi uokolewe kwa njia ya kumwamini Kristo Yesu.


Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


Wakati ule, kijana Samweli aliendelea kumutumikia Yawe, akiwa amevaa kizibao cha kitani.


Mutoto Samweli aliendelea kukomaa, akazidi kupendwa na Yawe na watu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan