4 Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.
Mutu wa hasira mbaya anasababisha ugomvi, lakini asiyekuwa mwepesi wa hasira anautuliza.
Kwa uvumilivu mutawala anaweza kusadikishwa; ulimi laini unavunja mifupa.
Kuna uovu niliotambua hapa chini ya jua, uovu unaosababishwa na watawala:
Usifanye haraka kukataa mamlaka yake, wala usiendelee kutenda lisilomupendeza, maana mufalme anafanya jinsi anavyopenda.