2 Moyo wa mwenye hekima unamwongoza kutenda mambo yanayokuwa sawa; lakini mutu mupumbafu anapotoshwa na moyo wake.
Hekima ya mwenye akili inamwonyesha njia yake, lakini upumbafu wa wapumbafu unawadanganya wenyewe.
Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.
Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?
Nguvu nyingi zaidi zinahitajika kwa mutumiaji wa shoka lisilonolewa, lakini kutumia hekima kunamufanya mutu afanikiwe.
Mupumbafu anasema maneno mengi. Mwanadamu hajui yatakayokuwa, wala yale yatakayotukia nyuma yake.
Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.
Ataweka kondoo kwa upande wake wa kuume, na mbuzi kwa upande wake wa kushoto.
Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.
Kwa kuwa mumefufuliwa pamoja na Kristo, mutafute mambo yanayokuwa juu, pahali Kristo anapoikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.