Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 10:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Chakula ni kwa ajili ya kujifurahisha, divai inachangamusha maisha, na feza inasababisha hayo yote.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 10:19
33 Iomraidhean Croise  

Chakula kilikuwa kikitwaliwa kutoka kwenye meza ya Yosefu na kupelekwa kwao, lakini Benjamina alipewa mara tano zaidi ya kipimo wandugu zake walichopewa. Basi, wakakunywa na kufurahi pamoja naye.


Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Mumwangalie Amunoni atakapokuwa amekunywa divai na kufurahi. Nitakapowaambia: ‘Mumupige Amunoni’, mumwue. Hiyo ni amri yangu kwenu. Mujipe moyo na mukuwe hodari.”


Lakini mufalme Daudi alimwambia Ornani: “Hapana; nitavinunua kwa bei yake kamili. Sitamutwalia Yawe kitu chako au kumutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto ambazo sikununua.”


Wajirani waliwasaidia watu hao kwa kuwapa vyombo vya feza, zahabu, mali, nyama na vitu vingine vya bei kali, mbali na vile vilivyotolewa kwa mapenzi.


Nikasema: “Kulingana na uwezo tunaokuwa nao, tumekuwa tukiwanunua tena wandugu zetu Wayuda waliokuwa wameuzishwa kwa watu wa mataifa mengine. Lakini sasa hata munawauzisha wandugu zenu, nasi tunalazimika kuwanunua!” Basi wakanyamaza kimya, bila kuwa na la kujibu.


Siku ya saba ya karamu hiyo, mufalme Ahasuero akiwa amejaa furaha kutokana na divai aliyokuwa amekunywa, akawaita matowashi saba waliomutumikia yeye mwenyewe: Mehumani, Bizita, Harbona, Bigita, Abagita, Zetari na Karkasi.


apate divai ya kumuchangamusha, mafuta ya muzeituni ya kumwangarisha, na mukate wa kumupa nguvu.


Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.


Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.


Kwenda ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo wenye kuchangamuka, maana Mungu amekwisha kukubali kazi yako.


Feza utakayopata itatakaswa kwa ajili ya Yawe. Hawatalinda feza hiyo lakini wale wanaomwabudu Yawe wataitumia kwa kununua chakula kingi na nguo nzuri.


Kuna kilio katika barabara kwa kukosa divai; shangwe yote imekoma, furaha imetoweka katika dunia.


Lakini haifai kuwakwaza. Kwa hiyo kwenda kwenye ziwa, na utupe ndoana ndani ya maji. Na samaki wa kwanza utakayemunasa, ufungue kinywa chake, nawe utaona kikoroti cha feza. Ukikamate na kukitoa kwa kulipa kodi kwa ajili yetu sisi wawili.”


Yesu akamujibu: “Ukitaka kuwa mutimilifu, kwenda uuzishe vitu unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate.”


Kisha nitajisemesha hivi juu yangu mwenyewe: ‘Uko na mali nyingi ulizoweka akiba kwa miaka mingi. Sasa utulizane, ukule na kunywa na kujifurahisha.’


Yesu akaongeza kusema: “Nami ninawaambia: mutumie mali ya dunia hii kwa kuunga urafiki, kusudi wakati mali ile itakapokosekana, mupate kupokelewa kwenye makao ya milele.


na Yoana muke wa Kuza, huyo mume wake alikuwa musimamizi wa mali ya Herode, pamoja na Suzana na wengine wengi. Wanawake hawa walitumia mali yao kwa kuwasaidia Yesu na wanafunzi wake.


Wanafunzi wakakusudia kutuma musaada kwa wandugu waamini waliokaa katika jimbo la Yudea, kila mumoja kwa kadiri alivyoweza kutoa.


Waliuzisha mali zao na vyote walivyokuwa navyo na kugawanya kati yao kufuatana na mahitaji ya kila mutu.


Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.


Baba yake akaenda katika nyumba ya yule binti, naye Samusoni akafanya karamu kule, kama vile vijana walivyofanya kwa wakati ule.


Lakini muzabibu ukajibu: ‘Munazani ninaweza kuacha shuguli yangu ya kuzalisha divai ambayo inafurahisha miungu na wanadamu, niende kujisumbua kuitawala miti?’


Abigaili aliporudi kwake, alimukuta Nabali akifanya karamu kubwa katika nyumba yake kama ya kifalme. Nabali alikuwa akifurahi sana ndani ya moyo maana alikuwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia neno lolote mpaka asubui.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan