18 Kutokana na uvivu wa mutu, paa ya nyumba inaanguka; kwa sababu ya uregevu, nyumba inavuja.
Kuwa na bidii kutamupa mutu cheo, lakini uvivu utamufanya mutumwa.
Mwanamuke mwenye hekima anajenga nyumba yake, lakini mupumbafu anaibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Muvivu halimi wakati wa kulima; wakati wa mavuno atatafuta lakini hatapata kitu.
Muvivu anakufa kwa kutokutimizwa kwa tamaa zake, maana mikono yake haitaki kufanya kazi.
maana walevi na walafi wataishia kuwa wamasikini. Usingizi utawavalisha nguo za kupasukapasuka.
Lakini tunatamani sana kwamba kila mumoja kati yenu aendelee kuonyesha bidii ile mpaka mwisho, kusudi mambo yale munayotumainia yapate kutimizwa.