Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 10:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Ole wako, ewe inchi, mutawala wako akiwa kijana, na viongozi wako wakifanya karamu asubui.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 10:16
16 Iomraidhean Croise  

Muzigo wa baba yangu ulikuwa muzito, lakini wangu utakuwa muzito zaidi. Baba yangu aliwapiga ninyi kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba.’ ”


Na watu wa ovyoovyo wakajiunga naye, watu wapumbafu wasiofaa kitu, nao wakamushawishi Rehoboamu mwana wa Solomono kutenda yale waliyotaka wao, naye hangeweza kuwazuia maana wakati ule alikuwa angali kijana bila mazoezi mengi.


Sedekia alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mumoja alipoanza kutawala, akatawala kule Yerusalema kwa muda wa miaka kumi na mumoja.


Yoahazi alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitatu alipoanza kutawala; akatawala kwa muda wa miezi mitatu akiwa kule Yerusalema.


Yoyakimu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano alipoanza kutawala, akatawala kwa muda wa miaka kumi na mumoja akiwa kule Yerusalema. Alitenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wake.


Yoyakini alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, alitawala kule Yerusalema kwa muda wa miezi mitatu na siku kumi. Alitenda maovu mbele ya Yawe.


Mutawala asiyekuwa na akili anawagandamiza sana watu, lakini anayechukia mali ya udanganyifu atatawala kwa muda murefu.


Mupumbafu anachokeshwa kwa kutoa jasho, hata hajui njia ya kwenda katika muji.


Watu wangu watateswa na watoto; wanawake ndio watakaowatawala. Enyi watu wangu, wakubwa wenu wanawapotosha, wanavuruga njia munayopaswa kufuata.


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan