Basi, nikatambua kwamba hakuna jambo linalokuwa bora zaidi kwa mwanadamu kufanya kuliko kufurahia kazi yake, kwa sababu amepangiwa hivyo. Nani anayeweza kumujulisha mwanadamu yale yatakayokuwa kisha kufa kwake?
Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?
Katika siku za kufanikiwa ukuwe na furaha. Katika siku za hasara ufikiri juu ya jambo hili: Mungu amefanya hiyo ya kwanza iambatane na ya pili kusudi mwanadamu asipate kujua mambo yatakayotukia nyuma yake.
Nilifikiri sana juu ya hayo yote, nikaona kwamba Mungu anaongoza matendo ya watu wenye hekima na wenye haki; ikiwa ni upendo au chuki, mwanadamu hajui. Kila kitu kwao ni bure,