Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nguvu nyingi zaidi zinahitajika kwa mutumiaji wa shoka lisilonolewa, lakini kutumia hekima kunamufanya mutu afanikiwe.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 10:10
20 Iomraidhean Croise  

Kwa hiyo, ninakuomba unipe mimi mutumishi wako moyo wa hekima nipate kuamua watu wako, niweze kutambua mazuri na mabaya; maana ni nani anayeweza kuhukumu watu wako wanaokuwa wengi hivi?”


Kutoka nusu ya kabila la Manase: watu elfu kumi na nane, waliotajwa majina kwa kuja kumuweka Daudi kuwa mufalme.


Nyoka ya muchawi ikiuma mbele haijachochewa, hakuna faida tena kwa muchawi.


Mupumbafu anachokeshwa kwa kutoa jasho, hata hajui njia ya kwenda katika muji.


Muchonga mawe anaumizwa nayo, mukata kuni anapatwa na hatari.


Basi, mimi nikagundua kwamba hekima ni bora kuliko upumbafu, kama vile mwangaza unavyokuwa bora kuliko giza.


Kuwa na hekima ni bora kuliko kutegemea silaha, lakini mwenye zambi mumoja anaharibu mazuri mengi.


“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.


Watu wote wanajua namna munavyomutii Bwana, na kwa sababu hii ninafurahi kwa ajili yenu. Lakini ninataka mukuwe wenye hekima kwa kutenda mema, na mukuwe safi mukijitenga na mambo mabaya.


Wandugu zangu, musikuwe kama watoto kwa kufikiri: lakini katika mambo mabaya, iwatokee kutenda kama watoto wachanga. Inafaa mafikiri yenu yakuwe kama ya watu wazima.


nitanoa upanga wangu unaometemeta, nitanyoosha mukono kutoa hukumu, nitawalipiza kisasi waadui zangu, nitawaazibu wale wanaonichukia.


Mukuwe na mwenendo wa hekima mbele ya watu wanaokuwa wa inje ya kanisa, mukitumia vema kila wakati munaoupata.


Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan