Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mwanadamu anafaidia nini kwa jasho lake lote hapa chini ya jua?

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 1:3
23 Iomraidhean Croise  

Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.


Nikachukia jasho yote niliyotoa hapa chini ya jua, kuona kwamba ilinipasa nimwachie mutu ambaye atatawala nyuma yangu.


Tena, ni nani anayejua kwamba atakuwa mwenye hekima au atakuwa mupumbafu? Hata hivyo, yeye atarizi yote niliyofanya kwa kutoa jasho na kutumia hekima yangu hapa chini ya jua. Hayo nayo ni bure.


Mutu anafaidia nini kutokana na jasho yake yote, na juhudi anazohangaika nazo chini ya jua?


Mufanya kazi anafaidia nini kutokana na jasho aliyotoa?


Lakini heri zaidi kuliko wafu na wanaokuwa wazima, yule ambaye bado hajazaliwa na kuona maovu yote yanayotendeka hapa chini ya jua.


Tena, niliona jambo moja la bure chini ya jua.


Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni, katika mahangaiko, magonjwa na hasira.


Kama Mungu anamupa mutu utajiri na mali na kumujalia wakati wa kuyafurahia, basi mwanadamu ashukuru na avifaidie hivyo alivyojipatia kwa jasho lake. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.


Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?


Hekima ni ya bei kubwa kama urizi; ni ya mafaa kwa wale wote wanaokuwa wazima.


Vilevile hapa chini ya jua nimeona mufano wa hekima, na ulionekana kwangu kuwa wenye maana sana.


Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.


Upendo wao, chuki zao na tamaa zao, vyote vimetoweka pamoja nao, wala hawatashiriki tena katika kitu chochote hapa chini ya jua.


Mbona munatumia feza zenu kwa ajili ya kitu kisichokuwa chakula? Kwa nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha? Munisikilize mimi kwa uangalifu, nanyi mutakula vinavyokuwa vitamu, na kufurahia vinavyokuwa bora.


Yawe wa majeshi anasababisha juhudi za watu zipotelee katika moto, na mataifa yajishugulishe bure.


Sanamu mutu aliyotengeneza inafaa kwa nini? Sanamu ni madini yaliyoyeyushwa, ni kitu cha kueneza udanganyifu! Mutengenezaji wa sanamu anatumainia kile alichotengeneza mwenyewe, sanamu ambayo haiwezi hata kusema!


Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake? Hakuna kitu mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.


Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”


mukubali kuongozwa na watu kama hawa na wale wote wanaotumika na bidii pamoja nao.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan