Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Mika 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Mika 1:2
33 Iomraidhean Croise  

Yawe anasema hivi: Sikiliza enyi mbingu, tega sikio ee dunia. Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha, lakini sasa wameniasi!


Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni. Kwa macho yake anawachungulia wanadamu, na kujua kila kitu wanachofanya.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa.”


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Lakini Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; dunia yote ikae kimya mbele yake.


Niliteremuka mpaka kwenye misingi ya milima, katika inchi ambayo milango yake imefungwa milele. Lakini wewe, ee Yawe, Mungu wangu, umenipandisha nikiwa muzima kutoka mule ndani ya shimo.


Ee inchi, ee inchi, ee inchi! Sikia neno la Yawe!


“Enyi watu wangu, munisikilize, mimi Mungu, Mungu wenu! Ninataka kusema nanyi. Israeli, ninakuonya.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoambia makanisa! “Yule atakayeshinda hatapatwa na kifo cha pili.


Munauliza: Mbona sasa hazikubali? Yawe hazikubali kwa sababu anajua wazi kwamba umeivunja ahadi yako kwa muke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.


Jambo hili litawafikia kwa sababu wametenda katika Israeli mambo yasiyofanyika. Walizini na wake za jirani zao, na kusema maneno ya uongo kwa jina langu, jambo ambalo mimi sikuwaamuru wafanye. Mimi ninajua hayo. Nimeyashuhudia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Sikiliza, ee dunia! Mimi nitawaletea watu hawa hasara kulingana na nia zao mbaya. Maana hawakuyajali maneno yangu, na mafundisho yangu nayo wameyakataa.


Kama ningesikia njaa, singekuambia wewe, maana ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vyangu.


Zaburi ya Asafu. Mungu, Mungu Yawe, amesema, amewaita wakaaji wa dunia, tokea magaribi mpaka mashariki.


Sikiliza sauti ya ombi langu, ninapokulilia unisaidie, ninapoinua mikono yangu kuelekea hekalu lako takatifu.


Zaburi ya Daudi. Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe; ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake.


Utege sikio, ee mbingu. Sikiliza, ee dunia, maneno ninayosema.


Wale wazee wa Gileadi wakamwambia Yefuta: “Yawe atakuwa mushuhuda kati yetu. Hakika tutafanya kama ulivyosema.”


Halafu Mikaya alisema: “Ukirudi salama basi, utajua kwamba Yawe hakusema nami.” Kisha akaendelea kusema: “Musikilize enyi watu wote!”


Mikaya akasema: “Ukirudi salama, basi, utajua kwamba Yawe hakusema nami.” Kisha akaendelea kusema: “Musikie, enyi watu wote!”


Enyi wakaaji wote katika ulimwengu, nanyi munaojaza dunia! Bendera itakaposimikwa kwenye mulima, muangalie! Baragumu itakapopigwa, musikilize.


Bwana wetu Yawe ananisaidia kwa hiyo siwezi kufazaika. Uso wangu nimeukaza kama jiwe; ninajua kwamba sitapata haya.


Kisha, watu wakamwambia Yeremia: Yawe akuwe mushuhuda wa kweli na mwaminifu juu yetu ikiwa hatutafanya jinsi Yawe, Mungu wako atakavyokuagiza utuambie.


“Enyi watu wote, ninawaita ninyi! Wito wangu ni kwa ajili ya wanadamu.


Roho yangu ilipoanza kunitoka, nilikukumbuka, ee Yawe, maombi yangu yakakufikia katika hekalu lako takatifu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan