Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Marko 8:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Basi Yesu akawaamuru watu waikae chini. Kisha akakamata ile mikate saba, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake waigawanye kwa watu; nao wanafunzi wakaigawanya.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Marko 8:6
18 Iomraidhean Croise  

Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Mutu yeyote anayeshugulika juu ya siku fulani, anafanya hivi kwa kumutukuza Bwana. Yule anayekula kila chakula, anafanya vile kwa kumutukuza Bwana; maana anamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula chake. Na asiyekula kila chakula anafanya hivi vilevile kwa kumutukuza Bwana na kumushukuru Mungu.


Na vilevile vyombo vingine vilivyotoka katika muji Tiberia vilifika karibu na pahali pale walipokula mikate, Bwana alipokuwa amekwisha kushukuru Mungu.


Halafu mama yake akawaambia watumishi: “Mufanye kila kitu atakachowaambia.”


Alipokuwa akiikaa kula chakula pamoja nao, akatwaa mukate na kuubariki. Kisha akaumega na kuwapatia.


Heri watumishi wale bwana wao atakaowakuta wakikesha wakati anapofika! Kweli ninawaambia: atafunga mukaba wake vizuri na kuwakaribisha kula chakula, na kubakia pale akiwashugulikia.


Walipokuwa wakikula, Yesu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema: “Mutwae na mukule, huu ni mwili wangu.”


Mara moja mutakapoingia katika muji, mutamukuta mbele hajakwenda kwenye nafasi ya ibada kwenye mulima kwa kula. Maana watu hawatakula mpaka kwanza yeye abariki sadaka. Kisha wale walioalikwa watakula. Hivyo muende haraka; mutakutana naye sasa hivi.”


Yesu akawauliza: “Muko na mikate ngapi?” Nao wakamujibu: “Tuko na mikate saba.”


Walikuwa vilevile na samaki ndogo chache. Yesu akamushukuru Mungu na kuwaambia wanafunzi wazigawanye vilevile.


Naye akawauliza tena: “Na wakati nilipomega mikate saba na kulisha watu elfu ine, mulijaza vitunga ngapi na vipande vya mikate?” Wakamujibu: “Saba.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan