Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.
Halafu Kuhani Mukubwa akapasua nguo zake na kusema: “Mutu huyu amemutukana Mungu! Hatuhitaji tena ushuhuda wowote juu yake. Angalia, munatoka kusikia jinsi alivyomutukana Mungu.
Walimu wa Sheria na Wafarisayo wakaanza kujiuliza: “Ni mutu gani huyu anayemutukana Mungu? Ni nani anayeweza kusamehe zambi, isipokuwa Mungu peke yake?”
Wayuda wakamujibu: “Hatutaki kukutupia mawe kwa ajili ya tendo zuri, lakini kwa sababu unamutukana Mungu. Wewe ni mutu tu, lakini unajifanya kuwa Mungu!”
Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?