“Hakuna mutu anayeshonea kiraka kipya juu ya nguo ya zamani. Kama anafanya vile, kile kiraka kipya kinapasua nguo ya zamani, na kupasuka kwake kunaongezeka zaidi.
Vilevile hakuna mutu anayetia divai mupya ndani ya machupa ya ngozi yenye kuzeeka. Kama akifanya vile, ile divai mupya itapasua machupa yale yenye kuzeeka, nayo divai na machupa vyote vinapotea bure. Lakini inafaa kutia divai mupya ndani ya machupa mapya ya ngozi.”
Yesu akawaambia mufano huu vilevile: “Hakuna mutu anayekata kiraka kwenye nguo mupya na kukishonea juu ya nguo ya zamani. Kama anafanya vile, atakuwa amepasua ile nguo mupya na kile kiraka cha nguo mupya hakitashikamana na nguo ya zamani.
Majaribu yale munayopata, ni yale yanayowapata watu wengine wote. Mungu hatawaachilia kujaribiwa kupita nguvu zenu, kwa maana yeye ni mwaminifu. Jaribu litakapowatokea, atawapatia nguvu ya kulivumilia, hata muweze kulishinda.