Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Marko 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yesu akamujibu: “Unaona majengo haya makubwa? Hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine; yote yatabomolewa.”

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Marko 13:2
10 Iomraidhean Croise  

Katika siku Hezekia alipokuwa mufalme wa Yuda, Mika wa Moreseti aliwatangazia watu wote kwamba Yawe wa majeshi alisema hivi: Sayuni utalimiwa kama shamba, Yerusalema utabaki mabomoko, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.


Basi! Kwa sababu yenu, Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalema lundo la makokoto, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Lakini Yesu akawaambia: “Munaona haya yote? Kweli ninawaambia: hapa hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine; yote yatabomolewa.”


“Kutakuwa siku vitu hivi munavyoona vitabomolewa, wala hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine.”


Kwa maana tumemusikia akisema kwamba huyu Yesu wa Nazareti ataharibu hekalu hili na kugeuza desturi tulizopokea toka kwa Musa.”


Lakini uache kiwanja kinachokuwa inje ya hekalu, usikipime kwa maana kimetolewa kwa watu wa mataifa mengine watakaokanyaga muji mutakatifu kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan