4 Hivi Yoane alitokea katika jangwa, akibatiza watu, akiwahubiri kwamba wageuke toka zambi zao, wabatizwe, na Mungu atawasamehe.
Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.
Waliungama zambi zao, naye Yoane aliwabatiza katika muto Yordani.
Watu wengi walitoka katika Yerusalema na katika jimbo lote la Yudea kwa kumwendea Yoane. Walikubali zambi zao, naye akawabatiza katika muto Yordani.
Upate kuwajulisha watu wake kwamba atawaokoa akisamehe zambi zao.
Yoane vilevile alikuwa akibatiza kule Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu kule kulikuwa maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.
Ninyi munajua mambo yaliyotokea katika Yudea yote, yakianzia katika jimbo la Galilaya nyuma ya mahubiri ya Yoane yaliyoelekea ubatizo.
Basi sasa, unangojea nini? Simama ubatizwe na kuondolewa zambi zako, ukiomba kwa jina la Bwana.’ ”