Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Maombolezo 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Waadui wamenyoosha mikono yao, wapate kukamata vitu vyake vyote vya bei kali. Kweli umeona watu wa mataifa wakiingia ndani ya hekalu, watu ambao Yawe aliwakataza kuingia kati kusanyiko lake.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Maombolezo 1:10
22 Iomraidhean Croise  

Alitwaa vyombo vyote vya nyumba ya Mungu vikubwa na vidogo na hazina ya nyumba ya Yawe na ya mufalme na wakubwa wake. Alivipeleka vyote mpaka Babeli.


Katika siku ile ya sherehe, kitabu cha Musa kikasomwa na ikajulikana kwamba Waamoni na Wamoabu hawaruhusiwi kuingia katika mukutano wa watu wa Mungu.


Sisi watakatifu wako tulirizi inchi kwa muda kidogo tu, lakini waadui zetu wakakuja wakaharibu hekalu lako.


Yawe anasema: Nitazifanya mali zenu na akiba zenu zitekwe tena, wala hamutapewa malipo yoyote ya vitu hivyo kwa sababu ya zambi zenu zote mulizozitenda kila pahali katika inchi.


Zaidi ya hiyo, utajiri wote wa muji, mapato yake yote, vitu vyake vyote vya bei kali pamoja na akiba zote za wafalme wa Yuda, nitavitoa katika mikono ya waadui, ambao watavinyanganya na kuvipeleka Babeli.


Kwa maana Yawe wa majeshi anasema hivi juu ya nguzo, birika la shaba na misingi ya kuliwekea, vinara na vyombo vingine vilivyoachwa katika muji huu,


Kweli, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya vile vyombo vilivyoachwa katika nyumba ya Yawe, katika nyumba ya mufalme wa Yuda na katika Yerusalema:


Sikiliza! Wakimbizi na wenye kutoroka kutoka inchi ya Babeli wanakuja kutangaza huko Sayuni jinsi Yawe, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.


Ninyi munasema: Tumepatishwa haya na kutukaniwa; haya imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia katika sehemu takatifu za nyumba ya Yawe.


Aliteketeza kwa moto nyumba ya Yawe, nyumba ya kifalme na nyumba zote za Yerusalema; kila nyumba kubwa ilichomwa kwa moto.


Unapokuwa sasa mabomoko matupu, Yerusalema unakumbuka utukufu wake. Ulipoangukia katika mikono ya waadui zake, hakuna aliyekuwa pale kwa kuusaidia. Washindi wake walichekelea kuanguka kwake.


Mumelichafua hekalu langu kwa kuruhusu waingie humo watu wasiotahiriwa, watu wasionitii mimi, wakati mafuta na damu vinatolewa kwa ajili yangu. Hivyo, ninyi watu wangu mumelivunja agano langu kwa machukizo yenu yote.


Nitageuza uso wangu usiwaelekee; nitaachilia hekalu langu lichafuliwe. Wanyanganyi wataingia humo ndani na kulichafua.


Akawaambia: Muchafue nyumba ya Yawe kwa kuvijaza viwanja vyake maiti, kisha musonge mbele. Basi, wakaenda, wakawaua watu katika muji.


“Lakini mutamwona yule anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ akisimamishwa pahali asipopaswa kuwa. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake). Basi watakaokuwa Yudea, wakimbilie kwa milima.


“Na mwana haramu yeyote, wala muzao wake hata kizazi cha kumi, haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe.


“Mwamori au Mumoabu yeyote, wazao wao wote hata kizazi cha kumi, hawaruhusiwi kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe,


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan