Kisha Paulo na wenzake wakaingia ndani ya chombo, wakaondoka katika muji Pafo na kwenda katika muji Perga katika jimbo la Pamfilia. Walipofika kule Yoane aliyeitwa vilevile Marko akaachana nao na kurudi Yerusalema.
Fujo ikajaa katika muji wote. Wale watu wakawakamata wanainchi wa Makedonia, Gayo na Aristarko waliokuwa wakisafiri pamoja na Paulo. Nao wote pamoja wakawapeleka kwa haraka katika nyumba ya makutano.
Tukapanda ndani ya chombo kilichotoka Adramiti, kilichokuwa tayari kupitia kwenye vivuko vya jimbo la Azia. Halafu tukaondoka tukiwa pamoja na mwanainchi mumoja wa Makedonia aliyeitwa Aristarko, wa Tesalonika.
Kwa ngambo ya Tito, yeye ni mwenzangu, ninafanya kazi pamoja naye kwa ajili yenu. Nao wale wandugu wengine wanaomusindikiza, ni wajumbe wa makanisa wanaotumika kwa ajili ya utukufu wa Kristo.
Niliona vema kuwatumia ndugu yetu Epafrodito, anayeshiriki pamoja nami katika kazi na katika vita ya Habari Njema. Ni yeye ndiye muliyetumia kwa kunisaidia kufuatana na mahitaji niliyokuwa nayo.
Na wewe vilevile mutumishi mwenzangu mwaminifu, ninakuomba uwasaidie wanawake hao, kwa maana walisumbuka sana pamoja nami katika kazi ya kutangaza Habari Njema. Kuko vilevile Klementi na wenzangu wengine wa kazi. Hao wote majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.