Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Filemono 1:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Vilevile Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanya kazi wenzangu, wanakusalimia.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Filemono 1:24
15 Iomraidhean Croise  

Alipokwisha kufahamu mambo yale yaliyotokea, akaenda kwa Maria, mama ya Yoane aliyeitwa Marko. Watu wengi walikuwa wamekusanyika mule, wakiomba.


Barnaba na Saulo walipomaliza kazi yao, wakarudi toka Yerusalema, wakiwa pamoja na Yoane, aliyeitwa vilevile Marko.


Kisha Paulo na wenzake wakaingia ndani ya chombo, wakaondoka katika muji Pafo na kwenda katika muji Perga katika jimbo la Pamfilia. Walipofika kule Yoane aliyeitwa vilevile Marko akaachana nao na kurudi Yerusalema.


Fujo ikajaa katika muji wote. Wale watu wakawakamata wanainchi wa Makedonia, Gayo na Aristarko waliokuwa wakisafiri pamoja na Paulo. Nao wote pamoja wakawapeleka kwa haraka katika nyumba ya makutano.


Tukapanda ndani ya chombo kilichotoka Adramiti, kilichokuwa tayari kupitia kwenye vivuko vya jimbo la Azia. Halafu tukaondoka tukiwa pamoja na mwanainchi mumoja wa Makedonia aliyeitwa Aristarko, wa Tesalonika.


Kwa ngambo ya Tito, yeye ni mwenzangu, ninafanya kazi pamoja naye kwa ajili yenu. Nao wale wandugu wengine wanaomusindikiza, ni wajumbe wa makanisa wanaotumika kwa ajili ya utukufu wa Kristo.


Niliona vema kuwatumia ndugu yetu Epafrodito, anayeshiriki pamoja nami katika kazi na katika vita ya Habari Njema. Ni yeye ndiye muliyetumia kwa kunisaidia kufuatana na mahitaji niliyokuwa nayo.


Na wewe vilevile mutumishi mwenzangu mwaminifu, ninakuomba uwasaidie wanawake hao, kwa maana walisumbuka sana pamoja nami katika kazi ya kutangaza Habari Njema. Kuko vilevile Klementi na wenzangu wengine wa kazi. Hao wote majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.


Mufungwa mwenzangu Aristarko anawasalimia. Naye Marko, binamu wa Barnaba anawasalimia vilevile. (Mumekwisha kupata maagizo juu ya Marko; akifika kwenu mumupokee vizuri).


Luka, muganga wetu mupendwa na Dema wanawasalimia.


Kanisa linalokuwa katika Babeli, lililochaguliwa na Mungu kama vile ninyi, linawasalimia. Vilevile Marko, mwana wangu katika imani, anawasalimia.


Basi sisi tunapaswa kuwasaidia watu kama hawa tupate kushiriki pamoja nao katika kazi ya kutangaza ukweli.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan