Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Filemono 1:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini sikutaka kufanya kitu chochote pasipo shauri lako. Wala sikutaka kukulazimisha unitendee mema; lakini ningetaka uyatende kwa mapenzi yako mwenyewe.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Filemono 1:14
10 Iomraidhean Croise  

Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe unapima moyo, nawe unapendezwa na uaminifu. Nami, katika uaminifu wa moyo wangu nimetoa vitu hivi vyote kwa mapenzi yangu, na sasa ninaona watu wako wanaokuwa hapa, wakikutolea kwa mapenzi yao na furaha.


Watu wako watajitolea, siku utakapokwenda kuwapiga waadui. Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia, kama umande unaotokeza asubui mapema.


Ingekuwa nimechagua kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe, ningeweza kungojea kupokea mushahara. Lakini kwa kuwa ni muzigo niliopewa, inanipasa kuitimiza.


Ni askari gani anayejilipia mwenyewe vifaa vya kiaskari? Au ni muchungaji gani asiyekunywa maziwa ya kundi analochunga?


Hatutafuti kuwaamuru ninyi juu ya mambo yale munayopaswa kuamini, maana munasimama imara katika imani. Lakini tunataka kutumika pamoja nanyi kusudi mupate kufurahi.


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Ni hivi niliona kuwa ni vizuri kuwashauri wandugu hawa watangulie kufika kwenu mbele yangu kusudi watayarishe vile vitu mulivyoahidi kutoa kwa mapenzi yenu. Hivi vitakuwa tayari na itaonyesha kwamba mumevitoa kwa moyo mwema, wala si kwa uchoyo.


Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan