Esteri 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20023 Malkia Esteri akamujibu: “Kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ewe mufalme, na ikikupendeza kunitimizia ombi langu, hitaji yangu ni mimi niishi na watu wangu vilevile. Faic an caibideil |
Kwa mara ingine tena, mufalme akatuma kiongozi mwingine na watu wake makumi tano. Kiongozi wa tatu akapanda kwenye mulima, akapiga magoti mbele ya Elia na kumusihi akisema: “Ewe mutu wa Mungu, ninakusihi uyahesabu maisha yangu na maisha ya hawa watumishi wako makumi tano yakuwe ya bei kali mbele yako.
“Ikikupendeza, ewe mufalme, na kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ukiona ni vizuri nami nikikupendeza, tafazali, toa tangazo la kuvunja mipango ambayo Hamani alikuwa ameamuru itimizwe. Mipango hiyo ni ile ya mwana wa Hamedata, wa uzao wa Agagi, aliyopanga kwa kuwaangamiza Wayuda wote katika majimbo yote.