Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakubwa wetu, babu zetu na taifa letu lote.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 9:6
29 Iomraidhean Croise  

kwa sababu Waisraeli hawakutii sauti ya Yawe, Mungu wao, lakini walivunja agano lake, hata hawakusikia wala kutii yote Musa, mutumishi wa Yawe, aliyowaamuru.


Yawe akamwonya Manase na watu wake, lakini hawakumusikia.


Tangu nyakati za babu zetu mpaka sasa, sisi watu wako tumekukosea sana. Na kwa sababu ya zambi zetu, sisi, wafalme wetu na makuhani wetu tulitiwa katika mikono ya wafalme wa inchi za kigeni, tukauawa, tukapelekwa kuwa wafungwa na kunyanganywa mali zetu. Na hata hivi leo, tumetiwa haya kupita kiasi.


Ukawavumilia kwa miaka mingi, na kuwaonya kwa njia ya roho wako kwa kupitia manabii wako; hata hivyo hawakusikiliza. Basi ukawaacha ukawatia katika mikono ya mataifa mengine.


Kwa hiyo, ee Mungu wetu, Mungu mukubwa, mwenye nguvu na wa kutisha, wewe unashika agano lako na kutenda wema. Mateso yaliyotupata, sisi, wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu, manabii wetu, babu zetu na watu wako wote tangu wakati wa wafalme wa Asuria mpaka leo, usiyaone kuwa ni madogo.


Wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu na babu zetu hawakushika Sheria yako wala kujali amri zako na maonyo yako uliyowapa.


na kuyajali maneno ya watumishi wangu manabii ambao ninawatuma kwenu kila mara, ingawa hamukuwasikiliza,


Nitafanya hivyo kwa sababu hamukusikiliza maneno yangu niliyowaambia kila mara kwa njia ya watumishi wangu, manabii, nanyi mukakataa kusikiliza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Juu ya neno ulilotuambia kwa jina la Yawe, hatutakusikiliza.


Ninyi mumefanya mambo hayo yote. –Ni ujumbe wa Yawe.– Na hata niliposema nanyi tena na tena hamukunisikiliza. Nilipowaita hamukuitika.


Lakini wao hawakunitii wala kunitegea sikio. Lakini wakafuata mashauri yao wenyewe na ugumu wa mioyo yao, wakarudi nyuma pahali pa kusonga mbele.


Tulikataa kukusikiliza, ee Bwana wetu, Mungu wetu; hatukutenda kulingana na sheria zako ulizotupatia kwa njia ya watumishi wako manabii.


Wewe, Bwana Mungu wetu, una huruma na musamaha, ingawa sisi tumekuasi.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema. Wewe unaua manabii na kuwatupia mawe wale ambao Mungu anakutumia. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Wakaaji wa Yerusalema na wakubwa wao hawakumutambua Yesu wala maandiko ya manabii yaliyosomwa kila siku ya Sabato. Lakini ingawa hivi wakatimiza maandiko yale kwa njia ya kumuhukumu kufa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan