Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 9:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 9:25
32 Iomraidhean Croise  

Kisha mufalme akamwambia Zadoki: “Urudishe Sanduku la Agano la Mungu katika muji. Kama nimepata kukubaliwa mbele ya Yawe, bila shaka atanirudisha na kunijalia kuliona tena Sanduku lake na kuyaona makao yake.


Kazi ya kuijenga upya nyumba ya Mungu katika Yerusalema ilisimama, na hali hiyo ikaendelea mpaka mwaka wa pili wa utawala wa Dario, mufalme wa Persia.


Nyuma ya mambo yale, wakati wa utawala wa mufalme Artasasta wa Persia, kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Ezra. Ezra alikuwa mwana wa Seraya mwana wa Azaria mwana wa Hilkia


Wakafika Yerusalema katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano katika mwaka wa saba wa utawala wa mufalme Artasasta.


Basi Eliasubu, Kuhani Mukubwa, pamoja na wandugu zake waliokuwa makuhani wakasimama na kuanza kujenga Mulango wa kondoo. Wakautakasa na kutia milango yake; wakaitakasa tangia kwenye Munara wa Mia Moja mpaka Munara wa Hananeli.


Kwa hiyo wakafanya shauri baya kwa kuja pamoja Yerusalema kutushambulia na hivyo kuleta muvurugano katika muji ule.


Nilipoona kwamba watu walikuwa na hofu nikawaambia wakubwa, wasimamizi na watu wote kwa jumla: “Musiwaogope hata kidogo. Mukumbuke Bwana anayekuwa mukubwa na wa kutisha, basi mupigane kwa ajili ya wandugu zenu, wana wenu, wabinti zenu, wake zenu na nyumba zenu.”


Basi, ukuta ikamalizika siku ya makumi mbili na tano ya mwezi wa Eluli; nayo ilidumu muda wa siku makumi tano na mbili.


Maana waadui zangu wanasema vibaya juu yangu; wanaovizia maisha yangu wanafanya mipango,


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Pembe dogo ile ikajitukuza mbele ya mukubwa wa viumbe vya mbinguni. Ikakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto ambazo mukubwa wa viumbe vya mbinguni alivyotambikiwa kila siku, na kuchafua hekalu lake.


Kwa werevu wake, atafanikiwa katika mipango yake ya udanganyifu, naye atajitukuza. Atawaangamiza watu wengi sana, na atataka kupigana na Mukubwa wa wakubwa, lakini ataangamizwa pasipo kutumia nguvu za kimutu.


Ulipoanza kuomba, Mungu alitoa jibu, nami nimekuja kukuelezea jibu hilo kwa sababu unapendwa sana. Kwa hiyo, usikilize kwa uangalifu jibu hilo na kuelewa maono hayo.


Yawe anasema hivi: Lakini wewe Betelehemu katika Efurata, wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda, lakini kwako kutanitokea mutawala atakayetawala juu ya Israeli. Asili yake ni ya zamani sana.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika udongo muzuri ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu na kulielewa. Nao wanazaa matunda; wamoja matunda mia moja, wengine makumi sita na wengine makumi tatu.”


“Mutamwona yeye anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ yule aliyetajwa na nabii Danieli, akisimamishwa katika hekalu. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake.)


“Lakini mutamwona yule anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ akisimamishwa pahali asipopaswa kuwa. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake). Basi watakaokuwa Yudea, wakimbilie kwa milima.


Andrea alimukuta kwanza Simoni, ndugu yake wa tumbo na kumwambia: “Tumemwona Masiya” (maana yake “Kristo”).


Mwanamuke yule akamwambia: “Ninajua kwamba Masiya anayeitwa Kristo, atakuja. Na wakati atakapokuja atatuelezea maneno yote.”


Halafu mukamwua yule anayekuwa asili ya uzima, lakini Mungu amemufufua. Na sisi ni washuhuda wa jambo hilo.


Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.


Filipo akaenda mbio karibu na gari, naye akamusikia yule mukubwa akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Filipo akamwuliza: “Unaelewa maneno unayoyasoma?”


Mutumie vema wakati huu munaokuwa nao kwa maana siku hizi ni mbaya.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


Na juu ya nguo yake na paja la muguu wake kulikuwa kumeandikwa jina hili: “Mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan