Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”
Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?
Na kadiri nilivyokuwa mwangalifu kuwaongoa, kuwabomoa, kuwaangusha, kuwaharibu na kuwatesa, ndivyo nitakavyokuwa mwangalifu kwa kuwapanda na kuwajenga. –Ni ujumbe wa Yawe.
Mimi ninawachungulia hao si kwa mema lakini kwa mabaya. Watu wote wa Yuda katika inchi ya Misri wataangamizwa kwa upanga na njaa, hakutabaki hata mutu mumoja.
Wewe umesahau yale ambayo mimi nilikufanyia ulipokuwa kijana. Wewe umenichukiza sana kwa mambo yale yote. Basi, nitakulipiza kisasi juu ya kila kitu ulichotenda. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Haukuongeza uchafu juu ya machukizo yako yote?
Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.
Kwako, ee Bwana, kuna haki, lakini sisi tumepata haya siku zote. Jambo hili ni kweli kwetu sisi wote tunaoishi Yudea, wakaaji wa muji Yerusalema na Waisraeli wote ambao umewatawanya katika inchi za mbali na za karibu kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.