Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 9:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kwa hiyo, ee Yawe, Mungu wetu, ulikuwa tayari kutuazibu, na ukafanya hivyo, kwa sababu unafanya mambo yanayokuwa ya haki, nasi hatukukusikiliza.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 9:14
16 Iomraidhean Croise  

Halafu wakubwa wa Israeli na mufalme wakajinyenyekeza, wakasema: “Yawe ni mwenye haki.”


Ee Yawe, Mungu wa Israeli, wewe ni mwenye haki na umetuacha tubaki kama vile tunavyokuwa hivi leo. Tunaungama makosa yetu mbele yako, tukijua kwamba hakuna anayekuwa na haki yoyote ya kuja mbele yako kwa ajili ya makosa haya.”


Hata hivyo, una haki kwa kutuazibu hivyo; maana wewe umekuwa mwaminifu wakati sisi tumekuwa watenda maovu.


Matendo yake ni ya haki na ya kuaminika; kanuni zake zote ni za kutegemewa siku zote.


Yawe ni mwenye huruma na haki; Mungu wetu ni mwenye rehema.


Ee Yawe, wewe ni wa haki; na hukumu zako ni za usawa.


Unirudishie furaha ya wokovu wako, uniimarishe kwa Roho wako mwema.


Basi, mufalme wa Misri akaagiza Musa na Haruni waitwe, akawaambia: “Mara hii nimetenda zambi. Yawe ana haki na mimi na watu wangu tumekosa.


Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?


Na kadiri nilivyokuwa mwangalifu kuwaongoa, kuwabomoa, kuwaangusha, kuwaharibu na kuwatesa, ndivyo nitakavyokuwa mwangalifu kwa kuwapanda na kuwajenga. –Ni ujumbe wa Yawe.


wanauzunguka Yerusalema kama walinzi wanavyozunguka mashamba, kwa sababu watu wake wameniasi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mimi ninawachungulia hao si kwa mema lakini kwa mabaya. Watu wote wa Yuda katika inchi ya Misri wataangamizwa kwa upanga na njaa, hakutabaki hata mutu mumoja.


Waadui zake ndio wanaoutawala na wanafanikiwa, maana Yawe ameutesa kwa sababu ya makosa yake mengi. Watoto wake wanapelekwa katika uhamisho.


Wewe umesahau yale ambayo mimi nilikufanyia ulipokuwa kijana. Wewe umenichukiza sana kwa mambo yale yote. Basi, nitakulipiza kisasi juu ya kila kitu ulichotenda. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Haukuongeza uchafu juu ya machukizo yako yote?


Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.


Kwako, ee Bwana, kuna haki, lakini sisi tumepata haya siku zote. Jambo hili ni kweli kwetu sisi wote tunaoishi Yudea, wakaaji wa muji Yerusalema na Waisraeli wote ambao umewatawanya katika inchi za mbali na za karibu kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan