Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 9:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Umetuazibu kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, lakini mpaka sasa, ee Yawe, Mungu wetu, hatukuomba musamaha wako kwa kuziacha zambi zetu na kutambua uaminifu wako.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 9:13
35 Iomraidhean Croise  

Yawe anasema hivi: Nitaleta uovu juu ya pahali hapa na juu ya wakaaji wake kama vile inavyokuwa katika kitabu kilichosomwa na mufalme wa Yuda.


Waovu wanapenda kukasirika; hawamwombi musaada anapowafunga.


Uyafungue macho yangu, nipate kuona maajabu ya sheria yako.


Unifundishe namna ya kushika kanuni zako, nami nitafikiri juu ya matendo yako ya ajabu.


Kwa mikono yako wewe mwenyewe uliniumba; unijalie akili nijifunze amri zako.


Umezuia kasirani yako yote; umeacha hasira yako kali.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Mambo niliyotabiri yametukia; na sasa ninatangaza mambo mapya, ninakuelezea hayo mbele hayajatukia.


Lakini ewe taifa la Yakobo, haukuniabudu mimi; enyi watu wa Israeli, mulichoka nami!


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Yawe atakata katika Israeli kichwa na mukia, tawi la mingazi na nyasi, kwa muda wa siku moja tu.


Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.


Wapenzi wako wote wamekusahau; hawajali kitu chochote juu yako. Nimekupiga sawa vile ungekuwa adui yangu. Umeazibiwa bila huruma, kwa sababu kosa lako ni kubwa, zambi zako ni nyingi sana.


Nimesikia Efuraimu akilalamika hivi: Umeniazibu vikali, maana nilikuwa kama mwana-ngombe asiyezoea nira. Unigeuze nami nitakugeukia, maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wangu.


Hasara hizi zimewapata mpaka leo kwa sababu muliitolea miungu mingine sadaka za kuteketezwa na kumukosea Yawe, mukakataa kusikiliza sauti yake au kufuata sheria yake, masharti yake na maagizo yake.


Mimi ninawachungulia hao si kwa mema lakini kwa mabaya. Watu wote wa Yuda katika inchi ya Misri wataangamizwa kwa upanga na njaa, hakutabaki hata mutu mumoja.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Utugeuze, ee Yawe, kusudi tukurudilie. Uturudishie hali ya zamani.


Wewe umesahau yale ambayo mimi nilikufanyia ulipokuwa kijana. Wewe umenichukiza sana kwa mambo yale yote. Basi, nitakulipiza kisasi juu ya kila kitu ulichotenda. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Haukuongeza uchafu juu ya machukizo yako yote?


Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwangiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutumishi wako.


Kiburi cha Waisraeli kinawashuhudia wao wenyewe, hawanirudilii mimi Yawe, Mungu wao; wala hawanitafuti kwa ajili ya matukio hayo yote.


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Wote wamewaka hasira kama furu, na wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wao wote wameanguka, wala hakuna anayeniomba musaada.


Halafu akawafungua akili kusudi wapate kufahamu Maandiko Matakatifu


Maandiko Matakatifu hayawezi kuvunjwa. Mungu aliwaita ‘miungu’ wale walioambiwa neno lake.


Imeandikwa hivi katika maandiko ya manabii: ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Kila mutu anayemusikia Baba na kufuata mafundisho yake, anakuja kwangu.


Halafu mutajua ukweli, na ukweli utawaweka huru.”


Hakika mumesikia habari zake, nanyi mukiwa waamini mumefundishwa kufuatana na ukweli unaokuwa ndani ya Kristo.


“Kwa muda wa miaka makumi ine, mimi niliwaongoza katika jangwa, nguo zenu mulizovaa hazikuchakaa wala viatu vyenu havikuchakaa kwenye miguu yenu.


Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan