Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 8:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kwa hiyo yule beberu alijitukuza sana. Lakini alipofikia kilele cha nguvu zake, ile pembe yake kubwa ikavunjika. Pahali pake kukaota pembe ine zilizoonekana waziwazi, zikiwa zimeelekea pande ine za dunia.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 8:8
19 Iomraidhean Croise  

Lakini wakati mufalme Uzia alipokuwa na nguvu, moyo wake akajaa kiburi ambacho kilisababisha maangamizi yake. Akamwasi Yawe wake kwa kuingia ndani ya hekalu akikusudia kufukiza ubani juu ya mazabahu.


Mordekayi sasa akakuwa mutu mwenye madaraka makubwa katika nyumba ya kifalme, na habari zake zikaenea katika majimbo yote kwamba uwezo wake ulikuwa unazidi kuongezeka.


Nitaleta upepo kutoka pande zote za mbingu; nitawatawanya kila pahali, wala hakutakuwa taifa lolote ambalo halitakuwa na wakimbizi wa Elamu.


Kama vile kikapu kinachojaa ndege walionaswa, ndivyo nyumba zao zinavyojaa mali za udanganyifu. Ndiyo maana wamekuwa watu wakubwa na watajiri,


Uishi, na ukomae kama mumea katika shamba. Nawe ukakomaa na kurefuka hata ukakuwa binti. Maziba yako yakakomaa na nywele zako nazo zikarefuka. Lakini ulikuwa uchi kabisa.


Utaendelea kujiona kuwa mungu mbele ya hao watakaokuua? Katika mikono ya hao watakaokuangamiza, utatambua kwamba wewe ni mutu tu, wala si mungu!


Hata hivyo, wakati atakapokuwa na nguvu, ufalme wake utavunjika na kugawanyika katika sehemu ine kuelekea pande ine za mbingu. Wazao wake hawatatawala, wala ufalme hautakuwa katika mikono ya urizi aliotawala, kwa sababu ufalme wake utakamatwa na wengine.


Kwa mwisho wa ile miaka saba, mimi Nebukadneza niliinua macho yangu kuangalia juu mbinguni na akili zangu zikanirudilia. Nilimushukuru Mungu Mukubwa na kumuheshimu yeye anayeishi milele: Kwa sababu mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ufalme wake unadumu kwa vizazi vyote.


Lakini alipoanza kuwa na kiburi, akakuwa na roho ngumu na mwenye majivuno, aliondolewa katika kiti chake cha kifalme, akanyanganywa utukufu wake.


Mimi Danieli niliona maono usiku. Ilikuwa hivi: Upepo ulivuma juu ya bahari kubwa toka pande zote ine za mbinguni.


Nyuma ya mambo hayo, nikaona nyama mwingine. Huyu alikuwa kama chui mwenye mabawa mane ya ndege juu ya mugongo wake. Alikuwa na vichwa vine naye alipewa uwezo wa kutawala.


Ile pembe iliyovunjika na pahali pake kukaota pembe ine, ina maana kwamba ufalme huo mumoja utagawanyika kuwa falme ine, lakini falme hizo hazitakuwa na nguvu kama ule ufalme wa kwanza.


Nilipokuwa ninawaza juu ya jambo hili, niliona beberu mumoja kutoka upande wa magaribi akikuja mbio bila kugusa chini. Kati ya macho yake alikuwa na pembe moja kubwa sana.


Nilimwona akimusogelea yule kondoo dume. Alikuwa amemukasirikia sana yule kondoo dume, hivyo akamushambulia kwa nguvu na kuzivunja zile pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuweza kuvumilia. Aliangushwa chini na kukanyagwakanyagwa, wala hakuna yeyote kwa kumwokoa toka katika nguvu zake.


Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.


Halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, naye atakusanya watu wake aliowachagua kutoka katika dunia nzima.


Nitakapowapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali, kama vile nilivyowaapia babu zao, nao watakula, watashiba na kunenepa, halafu watageukia miungu mingine na kuitumikia. Watanizarau na kuvunja agano langu.


Kisha mambo yale, nikaona wamalaika wane wakisimama kwenye pembe ine za dunia, wakizuiza upepo toka pande ine za dunia, kusudi usivume juu ya dunia, wala juu ya bahari, wala juu ya muti wowote.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan