Nilipokuwa ninawaza juu ya jambo hili, niliona beberu mumoja kutoka upande wa magaribi akikuja mbio bila kugusa chini. Kati ya macho yake alikuwa na pembe moja kubwa sana.
Nilimwona akimusogelea yule kondoo dume. Alikuwa amemukasirikia sana yule kondoo dume, hivyo akamushambulia kwa nguvu na kuzivunja zile pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuweza kuvumilia. Aliangushwa chini na kukanyagwakanyagwa, wala hakuna yeyote kwa kumwokoa toka katika nguvu zake.