Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 8:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nilipoinua macho yangu, niliona kondoo dume amesimama kando ya muto huo. Kondoo huyo alikuwa na pembe mbili ndefu, lakini moja ilikuwa ndefu zaidi, nayo ilitokea nyuma ya ile ingine.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 8:3
25 Iomraidhean Croise  

Daudi akainua macho yake, akamwona yule malaika wa Yawe akisimama kati ya mbingu na dunia, naye akiinua upanga wake juu ya Yerusalema tayari kuangamiza. Halafu Daudi na wazee wote walikuwa wakivaa nguo ya gunia, wakaanguka uso mpaka chini.


Hivi ndivyo Kiro mufalme wa Persia anavyosema: Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote katika ulimwengu na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, huko Yuda.


Tena wakawalipa wakubwa wa serikali ya Persia kituliro kusudi wapinge kazi ya Wayuda. Wakaendelea kufanya hivyo muda wote wa utawala wa Kiro, mpaka wakati wa utawala wa Dario.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, mufalme Ahasuero akaandaa karamu kwa ajili ya viongozi na watumishi wake wa serikali, wakubwa wa majeshi ya Persia na Media, watu wenye heshima na wakubwa wa majimbo.


Ninawachochea Wamedi juu yao; watu ambao hawajali feza wala hawavutwi na zahabu.


Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.


Ndimi ninasema juu ya mufalme Kiro: Ni muchungaji niliyemuchagua kwa ajili yangu. Yeye atatimiza mipango yangu yote. Ndimi ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema utajengwa tena upya; na juu ya hekalu: Musingi wako utawekwa tena.


Yawe amezichochea roho za wafalme wa Wamedi, kwa maana amekusudia kuiangamiza Babeli. Kweli, hicho ndicho kisasi cha Yawe; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Munoe mishale yenu! Mutwae ngao!


Nikainua macho, nikamwona mutu anayevaa nguo za kitani naye alikuwa amejifunga mukaba wa zahabu safi kutoka Ufasi.


Nyuma yako kutafuata ufalme mwingine, lakini ufalme huo utakuwa zaifu. Huu utafuatwa na ufalme wa tatu unaofananishwa na shaba; huo utaitawala dunia yote.


Yeye anakomboa na kuokoa, anafanya miujiza na maajabu mbinguni na katika dunia, maana amemwokoa Danieli toka nguvu za simba.


Nyama wa pili alikuwa kama dubu ambaye upande wake mumoja ulikuwa umeinuka. Na katika kinywa chake alikuwa na mifupa mitatu ya mbavu aliyoishika kwa meno yake. Sauti ikamwambia: Simama, ukule nyama nyingi kadiri unavyoweza.


Katika maono haya, nilijikuta niko Susani, muji mukubwa wa jimbo la Elamu. Nilikuwa nimesimama kando ya muto Ulayi.


Yule kondoo dume uliyemwona mwenye pembe mbili, ni wafalme wa Media na Persia.


Katika maono mengine, niliona pembe ine.


Nilipoangalia tena niliona kitabu kinaruka katika anga.


Yule malaika aliyeongea nami alinikaribia, akaniambia: Inua macho uone kile kinachokuja.


Nilipoangalia, niliona wanawake wawili wanatokea; walikuwa wakirushwa na upepo, nao walikuwa na mabawa yenye nguvu kama ya korongo. Wanawake wale wakakiinua kile kikapu katika anga.


Niliona maono mengine tena. Niliona magari mane ya vita yakitoka katikati ya milima miwili ya shaba nyeusi.


akainua macho, akawaona Waisraeli wamepiga kambi kila kabila pahali pake. Kisha Roho ya Mungu ikamufikia,


Siku moja Yoshua alipokuwa karibu na muji wa Yeriko, aliona kwa rafla mutu mumoja akisimama mbele yake na upanga uliochomolewa katika mukono wake. Yoshua akamwendea, akamwuliza: “Wewe ni wetu au ni wa waadui zetu?”


Kisha nikaona nyama wa pili wa ajabu akitokea ndani ya udongo. Alikuwa na pembe mbili zinazokuwa kama za mwana-kondoo naye alikuwa akisema kama nyoka mukubwa.


Halafu nikaona Mwana-Kondoo akisimama katikati ya kiti cha kifalme chenye kuzungukwa na vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee, naye alionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba; ndizo roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan