Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 8:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Katika maono haya, nilijikuta niko Susani, muji mukubwa wa jimbo la Elamu. Nilikuwa nimesimama kando ya muto Ulayi.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 8:2
24 Iomraidhean Croise  

Wana wa Semu walikuwa Elamu, Asuri, Aripakisadi, Ludi na Aramu.


Kwa wakati ule, mufalme Amurafeli wa Sinari, mufalme Arioki wa Elasari, mufalme Kedorilaomeri wa Elamu na mufalme Tidali wa Goimu,


Hili ni simulizi la Nehemia mwana wa Hakalia. Ilitukia kwamba, nilipokuwa katika muji mukubwa wa Susani, katika mwezi wa Kisileu wa mwaka wa makumi mbili,


Kiti chake cha kifalme kilikuwa katika muji mukubwa Susani.


Amri ya mufalme ilipotangazwa, wabinti wengi wakapelekwa Susani, muji mukubwa, wakawekwa chini ya ulinzi wa Hegayi. Esteri naye, akapelekwa kwenye nyumba ya kifalme, akawekwa chini ya uangalizi wa Hegayi, yule mwangalizi wa wanawake.


Kwa amri ya mufalme, tangazo hili lilitolewa katika muji mukubwa wa Susani, nao wajumbe wakalitangaza katika majimbo yote. Mufalme na Hamani wakaikaa chini kwa kunywa wakati watu katika muji wa Susani wanafazaika.


Esteri akamujibu: “Adui yetu mukubwa na mutesaji wetu, ni huyu mwovu Hamani!” Hapo Hamani akashikwa na hofu mbele ya malkia na mufalme.


Mordekayi alipotoka katika nyumba kwa mufalme, akiwa amevaa nguo ya kifalme ya rangi ya mayungiyungi na nyeupe, koti la kitani safi la rangi nyekundu, na taji kubwa ya zahabu, muji wa Susani ukajaa shangwe na vigelegele.


Siku ileile, mufalme akajulishwa jumla ya watu waliouawa katika muji mukubwa wa Susani.


Siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari, Wayuda wakakusanyika tena, wakawaua watu mia tatu zaidi katika muji wa Susani. Lakini hawakunyanganya mali za watu.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.


wafalme wote wa Simuri, Elamu na Medi;


Kwa siku ya tano ya mwezi wa ine, mwaka wa makumi tatu, wakati nilipokuwa katikati ya wale watu waliopelekwa katika uhamisho, karibu na muto Kebari, mbingu zikafunguka, nikapata maono toka kwa Mungu.


Elamu nayo iko huko. Makaburi ya waaskari wake yanaizunguka. Wote waliuawa katika vita. Wakashuka kwenye inchi ya wafu, bila kujua Mungu. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima. Lakini sasa wanapata haya yao pamoja na wale wanaoshuka katika shimo kwa wafu.


Siku ya makumi mbili na ine ya mwezi wa kwanza, nilikuwa nimesimama kando ya muto Tigre.


Maono niliyoyaona mimi Danieli yaliniogopesha, nami nikafazaika.


Mimi Danieli niliona maono usiku. Ilikuwa hivi: Upepo ulivuma juu ya bahari kubwa toka pande zote ine za mbinguni.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Belsasari, mimi Danieli nikapata maono mengine zaidi ya maono yale ya kwanza.


Nilipoinua macho yangu, niliona kondoo dume amesimama kando ya muto huo. Kondoo huyo alikuwa na pembe mbili ndefu, lakini moja ilikuwa ndefu zaidi, nayo ilitokea nyuma ya ile ingine.


Kisha Yawe akawaambia: Musikilize maneno yangu, kama kuna nabii kati yenu, mimi Yawe ninajifahamisha kwake katika maono na kuongea naye katika ndoto.


Zamani Mungu alisema na babu zetu kwa njia ya manabii, mara nyingi na kwa namna nyingi.


Na katika maono yale, nikaona wale farasi pamoja na wale waaskari waliopanda juu yao. Waaskari wale walikuwa na ngao zenye rangi nyekundu kama moto na zingine za rangi ya samawi na ya kimanjano kama kiberiti. Vichwa vya farasi wale vilikuwa kama vichwa vya simba, na ndani ya vinywa vyao mulitoka moto, moshi na mawe ya viberiti.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan