Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 7:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Nilipokuwa nikiendelea kuangalia, nikaona viti vya kifalme viliwekwa hapo, kisha Muzee mumoja wa zamani sana akakuja, akaikaa. Alikuwa amevaa nguo nyeupe kama teluji; nywele zake zilikuwa kama sufu safi. Kiti chake cha kifalme kilikuwa ndimi za moto, na magurudumu ya kiti kile yalikuwa moto unaowaka.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 7:9
34 Iomraidhean Croise  

Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


Kisha Mikaya akasema: “Basi sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akikaa katika kiti chake cha kifalme na jeshi lake lote la mbinguni likisimama upande wake wa kuume na wa kushoto.


Unapenda haki na kuchukia uovu. Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupendelea kuliko wenzako; amekuweka kuwa mufalme kwa kukupakaa mafuta ya kufurahisha.


Mbele milima haijakuwa, mbele haujauumba ulimwengu, wewe ndiwe Mungu, milele na milele.


Kiti chako cha kifalme ni imara tangu zamani; wewe umekuwa mbele ya nyakati zote.


Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote,


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Nitaweka kiti changu cha kifalme huko Elamu na kumwangamiza mufalme wao pamoja na wakubwa wao. –Ni ujumbe wa Yawe!


Juu ya kitu hicho niliona kitu kimoja kinachofanana na kiti cha kifalme chenye rangi la jiwe la yakuti. Juu yake kulikuwa kunaikaa kitu kinachofanana na mutu.


Wakati wa maono haya usiku, niliona kiumbe kinachofanana na mwanadamu. Akakuja katika mawingu na kumwendea yule Muzee wa zamani sana. Akakaribishwa mbele yake.


Lakini yule Muzee wa zamani sana akainuka, akawapa haki watakatifu wa Mungu na wakati ulipotimia, hao watakatifu wakapewa ufalme.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Wewe si ndiwe Yawe, tangu zamani sana? Wewe ndiwe Mungu wangu, Mutakatifu wangu, usiyekufa. Ee Yawe, umewachagua Wakaldea watuhukumu! Ewe kimbilio letu, umewaimarisha kusudi watuazibu!


Na kule sura ya Yesu ikageuka wazi mbele yao. Uso wake ukangaa kama jua, nazo nguo zake zikametameta kama mwangaza.


Yeye aliangaa kama umeme na nguo yake ilikuwa nyeupe sana.


Nguo zake zikageuka nyeupe sana na kumetameta, wala katika dunia hakuna fundi wa kufua anayeweza kuziangarisha kama vile.


Lakini kwa sababu alikuwa nabii, alijua kwamba Mungu amemwahidi kwa kiapo kwamba atamutawalisha mumoja wa wazao wake kwa kurizi ufalme wake.


Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Ni yeye tu asiyeweza kufa na anayekaa katika mwangaza ambao mutu hawezi kukaribia. Hakuna mutu aliyemwona wala hakuna mutu anayeweza kumwona. Ndiye mwenye heshima na uwezo wa milele! Amina.


Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kutoka kwa Yesu Kristo na kuitangaza kwenu: Mungu ni mwangaza, na ndani yake hamuna giza hata kidogo.


Nywele zake zilikuwa nyeupe sana kama pamba na kama barafu, macho yake yalimetameta kama ndimi za moto.


Hivi mutakula nyama za miili ya wafalme, za majemadari, za watu wenye uwezo, nyama za farasi pamoja na za watu wanaopanda juu yao na nyama za watu wote wanaokuwa huru na za watumwa, wakubwa kama vile wadogo.”


Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.


Na mara moja nikashikwa na Roho wa Mungu. Nikaona kiti cha kifalme kimewekwa kule mbinguni na mutu mumoja alikuwa akiikaa juu ya kiti kile.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan