Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 7:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Nyama wa pili alikuwa kama dubu ambaye upande wake mumoja ulikuwa umeinuka. Na katika kinywa chake alikuwa na mifupa mitatu ya mbavu aliyoishika kwa meno yake. Sauti ikamwambia: Simama, ukule nyama nyingi kadiri unavyoweza.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 7:5
14 Iomraidhean Croise  

Elisha aligeuka, akawaangalia na kuwalaani kwa jina la Yawe. Dubu wawili wakatoka katika pori, wakawararua vijana makumi ine na wawili kati yao.


Afazali kukutana na dubu dike aliyenyanganywa watoto wake, kuliko kukutana na mupumbafu katika upumbafu wake.


Enyi nyama wote wakali, nanyi nyama wote wa pori, mukuje mukule.


Sasa nitakuelezea ule ukweli wa mambo haya. Wafalme wengine watatu wataitawala inchi ya Persia. Hao watafuatwa na mufalme wa ine ambaye atakuwa tajiri kuliko wale waliomutangulia. Wakati atakapopata nguvu kwa ajili ya utajiri wake, ataanza kuushambulia ufalme wa Ugriki.


Nyuma yako kutafuata ufalme mwingine, lakini ufalme huo utakuwa zaifu. Huu utafuatwa na ufalme wa tatu unaofananishwa na shaba; huo utaitawala dunia yote.


PERESI: ufalme wako umegawanywa kati ya Wamedi na Wapersi.


Nyama wa kwanza alikuwa kama simba, na alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikiwa ninamwangalia, mabawa yake yaliongolewa, naye akainuliwa na kusimama kwa miguu miwili kama mutu. Kisha, akapewa akili ya kimutu.


Nyuma ya mambo hayo, nikaona nyama mwingine. Huyu alikuwa kama chui mwenye mabawa mane ya ndege juu ya mugongo wake. Alikuwa na vichwa vine naye alipewa uwezo wa kutawala.


Nitawarukia kama dubu aliyenyanganywa watoto wake. Nitawararua vifua vyenu na kuwakula palepale kama simba; nitawararua vipandevipande kama nyama wa pori.


Yule nyama niliyemwona alifanana na chui. Miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba. Yule nyoka mukubwa akamupa uwezo wake pamoja na kiti chake cha kifalme na mamlaka makubwa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan