Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 7:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Nyama wa kwanza alikuwa kama simba, na alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikiwa ninamwangalia, mabawa yake yaliongolewa, naye akainuliwa na kusimama kwa miguu miwili kama mutu. Kisha, akapewa akili ya kimutu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 7:4
27 Iomraidhean Croise  

Saulo na Yonatani, watu wema na wa kupendeza. Katika maisha na kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, wenye nguvu kuliko simba.


ni nini sasa mutu ambaye ni kidudu, mwanadamu ambaye ni nondo tu!


Ee Yawe, simama sasa mwanadamu asishinde! Uyakusanye sasa hivi mataifa mbele yako, uyahukumu.


Yawe amewaacha watu wake, kama vile simba anavyoacha pango lake; inchi yao imekuwa jangwa tupu, kwa sababu ya vita na hasira kali ya Yawe.


Angalia! Adui anakuja akivuma kama mawingu. Magari yake ya vita ni kama zoruba, nao farasi wake wa vita wanaruka mbio kuliko tai. Ole kwetu! Tumeangamia!


Kama simba anavyotoka kwenye maficho yake, mwangamizaji wa mataifa ameanza kuja, anakuja kutoka pahali pake, kusudi aharibu inchi yenu. Miji yenu itabaki mabomoko matupu, bila kukaliwa na mutu yeyote.


Yawe anasema hivi: Taifa litaruka mbio juu ya Moabu, kama tai aliyekunjua mabawa yake.


Kama vile simba anavyochomoka kutoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla Waedomu toka katika inchi yao. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?


Waliotufuatilia walikuwa wepesi kuliko tai, walitukimbiza kwenye milima walituvizia katika jangwa.


Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kulikuwa tai mumoja mukubwa sana aliyekuwa na mabawa makubwa, yenye manyoya marefu mengi yenye rangi za kila aina. Tai yule aliruka mpaka kwenye mulima Lebanoni, akatua juu ya kilele cha muti wa mwerezi;


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Utaendelea kujiona kuwa mungu mbele ya hao watakaokuua? Katika mikono ya hao watakaokuangamiza, utatambua kwamba wewe ni mutu tu, wala si mungu!


Amekupa mamlaka juu ya wanadamu wote, nyama wa pori na ndege wote, popote kule wanapokuwa. Wewe ndiwe kile kichwa cha zahabu!


Wale nyama wengine walinyanganywa mamlaka yao, lakini wao wenyewe wakaachwa waendelee kuishi kwa muda fulani.


Nyama wa pili alikuwa kama dubu ambaye upande wake mumoja ulikuwa umeinuka. Na katika kinywa chake alikuwa na mifupa mitatu ya mbavu aliyoishika kwa meno yake. Sauti ikamwambia: Simama, ukule nyama nyingi kadiri unavyoweza.


“Nafasi yoyote kunapokuwa muzoga, ndipo tai wanapokusanyika.


“Yawe ataleta kutoka mbali taifa moja liwashambulie mbio kama tai, taifa ambalo hamujui luga yake.


Yule nyama niliyemwona alifanana na chui. Miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba. Yule nyoka mukubwa akamupa uwezo wake pamoja na kiti chake cha kifalme na mamlaka makubwa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan